
Subscribe ndio neno gumu zaidi kwa wabongo kuliko kutafuna jiwe kama ilivyo kwa Waingereza kutamka Mwanjelwa..husema Monjela
Pamoja na vionjo hivyo..kwenye Simba Day ya mwaka huu ntakuja na style tofauti ya kutambulisha wachezaji...njoo ushuhudie mwenyew..usingoje kuhadithiwa ni Jtano hii pale dimba la Taifa... #SimbaDay #KibingwaZaidi 🇵🇪🇵🇪
Serikali yatoa tamko kuadimika mafuta ya kula nchini
Waziri Kigwangalla atetea ununuzi wa ndege
Zitto Kabwe amshauri Job Ndugai
Bunge lataka tende zifutwe kodi mfungo wa Ramadhani
Mo Dewji afunguka jinsi anavyopiga pesa kupitia kilimo
Magari ya kifahari yameonekana jana katika mazishi ya bilionea Ivan Ssemwanga yaliyofanyika nyumbani kwao Kayunga jijini Kampala.
Ivan aliyekuwa mume wa Zari Hassan maarufu ‘Zarithebosslady’ ambaye kwa sasa ni mpenzi wa Diamond Platnumz, alifariki dunia wiki iliyopita baada ya kupata kiharusi na kuwa katika hali ya koma kwa wiki mbili mfululizo katika hospitali ya Steven Biko huko Pretoria nchini Afrika Kusini.
Gazeti la Uganda, Daily monitor linaripoti kuwa miongoni mwa magari hayo ni pamoja na yale ya marehemu likiwemo Hammer lenye jina la Ivan 9, yale ya vizito mbalimbali wa jiji la Kampala waliohudhuria mazishi hayo pamoja na gari la tajiri wa Tanzania Jack Pemba aina ya Audi lenye jina la A Pemba ambalo lilionekana kuwa la kifahari zaidi.
Katika hali ambayo haikuonekana kuwa ya kushangaza, baadhi ya waombolezaji walionekana wakiomba na kupewa fedha kutoka kwa matajiri mbalimbali waliohudhuria.
Hata hivyo kaburi la Ivan liliwekwa mafungu ya fedha chini ikiwa ni maandalizi ya kuuweka mwili wa bilionea huyo.
Mwili wa Ivan ambao uliwasili Uganda siku mbili zilizopita katika ndege kubwa iliyobeba watu 50, umezikwa katika makaburi ya familia pembeni ya kaburi la baba yake.
Credit - Mwananchi
Post A Comment: