WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amesema Serikali ya Awamu ya Tano imejipanga na kuhakikisha sekta ya mifuko ya jamii inaboreshwa na kwa kuzingatia hilo imelipa deni la zaidi ya Sh bilioni 722.7 lililokuwa likidaiwa na mifuko hiyo.


Waziri Mkuu Majaliwa alisema hayo jana katika Mkutano Mkuu wa Sita wa Wadau na Wanachama wa Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF) uliofanyika jijini Arusha, akieleza kuwa deni hilo ni kati ya madeni ya michango ya jumla ya Sh bilioni 964.2.

Alisema serikali inakamilisha uhakiki wa madeni ya miradi ya mifuko ili itoe hati fungani na katika kipindi kinachoishia Juni mwaka huu takwimu zinaonesha idadi ya wanachama imeongezeka hadi kufikia milioni 2.1.

Waziri Mkuu aliwaambia wanachama na wadau kuwa katika kubana matumizi Serikali ya Awamu ya Tano imehakikisha gharama za uendeshaji wa mifuko zinapungua kutoka asilimia 19 ya michango ya wanachama hadi kufikia asilimia 10 kwa mujibu wa kanuni za gharama za mifuko zilizotolewa na Mamlaka ya Usimamizi na Udhibiti wa Sekta ya Hifadhi ya Jamii (SSRA).

Alisema serikali imejipanga kuona nchi inapata maendeleo ya haraka kwa manufaa ya Watanzania wote katika kutekeleza Dira ya Maendeleo ya Taifa 2025 pamoja na Ilani ya Uchaguzi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), imelenga kuiwezesha nchi kuwa ya uchumi wa kati wenye kujengwa na viwanda ili kuchochea mageuzi ya kiuchumi na maendeleo ya watu na kupunguza umasikini.

Waziri Mkuu alifarijika kusikia kuwa NSSF imedhamiria kwenda na mwendo huo kwa kupanua wigo wa uwekezaji wake na kuelekeza katika viwanda jambo ambalo litaongeza ajira, kuongeza uzalishaji na kukuza uchumi wa jumla.

Alisema maamuzi hayo yataiwezesha NSSF na mifuko mingine kupata wanachama wapya na kukusanya michango zaidi na kuiwekeza ili kutimiza lengo lake la msingi la hifadhi ya jamii.

Alisema uamuzi wa NSSF na PPF kuungana ili kukabiliana na tatizo la sukari nchini kwa kujenga kiwanda cha sukari mkoani Morogoro eneo la Mkulazi kitakachoweza kuzalisha tani 200,000 kwa mwaka na kuajiri watu zaidi ya 100,000 huo ni moyo wa uzalendo ambao unafaa kuigwa na kila mtu na taasisi na kampuni mbalimbali nchini.

DOWNLOAD APP YETU YA SWAHIBA NEWS ILI UWEZE KUPATA HABARI ZOTE MOJA KWA MOJA KUPITIA SIMU YAKO YA MKONONI BILA KUINGIA KWENYE WEBSITE,KUDOWNLOAD BONYEZA HAPA  

ANDIKA MAONI YAKO HAPO CHINI
ads
Bonyeza HAPA kudownload applicationi ya SWAHILI NEWS kwenye simu yako ili kupata habari zetu Haraka
Share To:

SWAHIBA MEDIA STAFF

Habari , karibu katika mtandao wetu ili kuhabarika na stori zote za siku katika lugha yetu adhwim ya kiswahili, habarika wakati wote weka dunia kiganjani mwako na swahili news

Post A Comment: