
Subscribe ndio neno gumu zaidi kwa wabongo kuliko kutafuna jiwe kama ilivyo kwa Waingereza kutamka Mwanjelwa..husema Monjela
Pamoja na vionjo hivyo..kwenye Simba Day ya mwaka huu ntakuja na style tofauti ya kutambulisha wachezaji...njoo ushuhudie mwenyew..usingoje kuhadithiwa ni Jtano hii pale dimba la Taifa... #SimbaDay #KibingwaZaidi π΅πͺπ΅πͺ
Serikali yatoa tamko kuadimika mafuta ya kula nchini
Waziri Kigwangalla atetea ununuzi wa ndege
Zitto Kabwe amshauri Job Ndugai
Bunge lataka tende zifutwe kodi mfungo wa Ramadhani
Mo Dewji afunguka jinsi anavyopiga pesa kupitia kilimo
WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amesema Serikali ya Awamu ya Tano
imejipanga na kuhakikisha sekta ya mifuko ya jamii inaboreshwa na kwa
kuzingatia hilo imelipa deni la zaidi ya Sh bilioni 722.7 lililokuwa
likidaiwa na mifuko hiyo.
Waziri Mkuu Majaliwa alisema hayo jana katika Mkutano Mkuu wa Sita wa
Wadau na Wanachama wa Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF)
uliofanyika jijini Arusha, akieleza kuwa deni hilo ni kati ya madeni ya
michango ya jumla ya Sh bilioni 964.2.
Alisema serikali inakamilisha uhakiki wa madeni ya miradi ya mifuko
ili itoe hati fungani na katika kipindi kinachoishia Juni mwaka huu
takwimu zinaonesha idadi ya wanachama imeongezeka hadi kufikia milioni
2.1.
Waziri Mkuu aliwaambia wanachama na wadau kuwa katika kubana matumizi
Serikali ya Awamu ya Tano imehakikisha gharama za uendeshaji wa mifuko
zinapungua kutoka asilimia 19 ya michango ya wanachama hadi kufikia
asilimia 10 kwa mujibu wa kanuni za gharama za mifuko zilizotolewa na
Mamlaka ya Usimamizi na Udhibiti wa Sekta ya Hifadhi ya Jamii (SSRA).
Alisema serikali imejipanga kuona nchi inapata maendeleo ya haraka
kwa manufaa ya Watanzania wote katika kutekeleza Dira ya Maendeleo ya
Taifa 2025 pamoja na Ilani ya Uchaguzi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM),
imelenga kuiwezesha nchi kuwa ya uchumi wa kati wenye kujengwa na
viwanda ili kuchochea mageuzi ya kiuchumi na maendeleo ya watu na
kupunguza umasikini.
Waziri Mkuu alifarijika kusikia kuwa NSSF imedhamiria kwenda na
mwendo huo kwa kupanua wigo wa uwekezaji wake na kuelekeza katika
viwanda jambo ambalo litaongeza ajira, kuongeza uzalishaji na kukuza
uchumi wa jumla.
Alisema maamuzi hayo yataiwezesha NSSF na mifuko mingine kupata
wanachama wapya na kukusanya michango zaidi na kuiwekeza ili kutimiza
lengo lake la msingi la hifadhi ya jamii.
Alisema uamuzi wa NSSF na PPF kuungana ili kukabiliana na tatizo la
sukari nchini kwa kujenga kiwanda cha sukari mkoani Morogoro eneo la
Mkulazi kitakachoweza kuzalisha tani 200,000 kwa mwaka na kuajiri watu
zaidi ya 100,000 huo ni moyo wa uzalendo ambao unafaa kuigwa na kila mtu
na taasisi na kampuni mbalimbali nchini.
DOWNLOAD
APP YETU YA SWAHIBA NEWS ILI UWEZE KUPATA HABARI ZOTE MOJA KWA MOJA
KUPITIA SIMU YAKO YA MKONONI BILA KUINGIA KWENYE WEBSITE,KUDOWNLOAD
BONYEZA HAPA
ANDIKA MAONI YAKO HAPO CHINI
Post A Comment: