Waziri Mkuu wa zamani wa Ureno Antonio Guterres anatarajiwa kuwa Katibu Mkuu mpya wa Umoja wa Mataifa baada ya kupata hakikisho kutoka kwa wanachama watano wakudumu wa Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa.


Idhinisho hilo lisilo rasmi litathibitishwa leo Alhamisi katika kura rasmi, kabla ya kupelekwa katika mkutano mkuu kwa ajili ya kuchaguliwa kwa kauli moja.

Antonio Guterres ambaye ni balozi wa Umoja wa Mataifa, ametumika kama Kamishna mkuu katika shirika la Wakimbizi kwa miaka 10.

Iwapo ataidhinishwa, atashika nafasi hiyo mwaka mpya, muda ambao Katibu mkuu wa sasa Ban Ki Moon atastaafu.

Uteuzi wake huo umekuja licha ya jitihada zilizokuwa zikichiukuliwa kuweza kumpata Katibu Mkuu mpya wa Umoja wa Mataifa, Mwanamke.

DOWNLOAD APP YETU YA SWAHIBA NEWS ILI UWEZE KUPATA HABARI ZOTE MOJA KWA MOJA KUPITIA SIMU YAKO YA MKONONI BILA KUINGIA KWENYE WEBSITE,KUDOWNLOAD BONYEZA HAPA  

ANDIKA MAONI YAKO HAPO CHINI
ads
Bonyeza HAPA kudownload applicationi ya SWAHILI NEWS kwenye simu yako ili kupata habari zetu Haraka
Share To:

SWAHIBA MEDIA STAFF

Habari , karibu katika mtandao wetu ili kuhabarika na stori zote za siku katika lugha yetu adhwim ya kiswahili, habarika wakati wote weka dunia kiganjani mwako na swahili news

Post A Comment: