
Subscribe ndio neno gumu zaidi kwa wabongo kuliko kutafuna jiwe kama ilivyo kwa Waingereza kutamka Mwanjelwa..husema Monjela
Pamoja na vionjo hivyo..kwenye Simba Day ya mwaka huu ntakuja na style tofauti ya kutambulisha wachezaji...njoo ushuhudie mwenyew..usingoje kuhadithiwa ni Jtano hii pale dimba la Taifa... #SimbaDay #KibingwaZaidi 🇵🇪🇵🇪
Serikali yatoa tamko kuadimika mafuta ya kula nchini
Waziri Kigwangalla atetea ununuzi wa ndege
Zitto Kabwe amshauri Job Ndugai
Bunge lataka tende zifutwe kodi mfungo wa Ramadhani
Mo Dewji afunguka jinsi anavyopiga pesa kupitia kilimo
Mbunge wa Kinondoni jijini Dar, Maulid Mtulia (CUF) jana ametangaza kujiuzulu ubunge na kujivua uanachama wa Chama cha Wananchi CUF na kuhamia CCM.
Katika barua yake ya kujiuzulu, Mtulia amesema kuwa ameamua kufanya uamuzi huo leo Disemba 2, kwa utashi wake bila shinikizo la mtu yeyote.
Mtulia ameelezea sababu za kujiuzulu nafasi yake hiyo ya ubunge na kuhama chama kuwa imetokana na uzoefu alioupata kwa miaka miwili ya ubunge, na kusema “nimebaini kuwa Serikali ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) ambacho ni chama tawala inafanya kazi kubwa ya kutekeleza Ilani na imefanya vizuri katika mambo mengi ambayo sisi upinzani tuliahidi kuyatekeleza” alisema.
Aidha Mbunge huyo amesema kuwa nia yake ni kuwatumikia wananchi, na haoni sababu ya kuendelea kuwa upinzani na badala yake anaona ni vema aungane na juhudi za Serikali, kwa kumuunga mkono Rais Dk. John Magufuli katika kuwaletea wananchi maendeleo na kukabiliana na kero mbalimbali.
Mtulia amesema anawashukuru wananchi wa Jimbo la Kinondoni, kwa kumpa dhamana ya ubunge, katika uchaguzi mkuu uliopita na amewaahidi kuwa yupo tayari kuendelea kushirikiana nao katika maendeleo, akiwa katika uwanja mwingine wa siasa ambao ni Chama Cha Mapinduzi.
Post A Comment: