
Subscribe ndio neno gumu zaidi kwa wabongo kuliko kutafuna jiwe kama ilivyo kwa Waingereza kutamka Mwanjelwa..husema Monjela
Pamoja na vionjo hivyo..kwenye Simba Day ya mwaka huu ntakuja na style tofauti ya kutambulisha wachezaji...njoo ushuhudie mwenyew..usingoje kuhadithiwa ni Jtano hii pale dimba la Taifa... #SimbaDay #KibingwaZaidi π΅πͺπ΅πͺ
Serikali yatoa tamko kuadimika mafuta ya kula nchini
Waziri Kigwangalla atetea ununuzi wa ndege
Zitto Kabwe amshauri Job Ndugai
Bunge lataka tende zifutwe kodi mfungo wa Ramadhani
Mo Dewji afunguka jinsi anavyopiga pesa kupitia kilimo
KOCHA wa Simba, Joseph Omog, amewataka wachezaji wake kuongeza umakini kwenye mchezo wao wa leo dhidi ya wenyeji Mbeya City kwenye Uwanja wa Sokoine.
Akizungumza na gazeti la Nipashe, Omog, alisema kuwa umakini mdogo hasa kwa safu yake ya ulinzi ilipelekea timu hiyo kutoka sare ya bao 1-1 na Yanga hivyo amewataka wachezaji wake kuwa makini hasa wanapokuwa wanaongoza mchezo.
βKama benchi la ufundi kazi yetu tumeifanya, imebaki kazi ya wachezaji uwanjani, lakini tunataka kuona tunapata ushindi, tunapaswa kuwa makini kwa kila dakika uwanjani,β alisema Omog.
Alisema kuwa anaimani kubwa na ushindi kutokana na maandalizi waliyoyafanya.
βMatokeo ya nyuma yamepita sasa tunaangalia mbele, ligi ni ngumu lakini lazima tupambane ili kupata ushindi,β alisema Omog.
Baada ya mchezo wa leo, Simba inayodhaminiwa na kampuni ya Sportpesa itarejea Dar es Salaam kabla ya kurejea tena Mbeya Novemba 16 kucheza na Tanzania Prisons.
Simba inaongoza kwenye msimamo wa ligi ikiwa na pointi 16 sawa na Yanga Azam na Mtibwa lakini yenyewe ikiwa na uwiano mzuri wa magoli.
Post A Comment: