
Subscribe ndio neno gumu zaidi kwa wabongo kuliko kutafuna jiwe kama ilivyo kwa Waingereza kutamka Mwanjelwa..husema Monjela
Pamoja na vionjo hivyo..kwenye Simba Day ya mwaka huu ntakuja na style tofauti ya kutambulisha wachezaji...njoo ushuhudie mwenyew..usingoje kuhadithiwa ni Jtano hii pale dimba la Taifa... #SimbaDay #KibingwaZaidi 🇵🇪🇵🇪
Serikali yatoa tamko kuadimika mafuta ya kula nchini
Waziri Kigwangalla atetea ununuzi wa ndege
Zitto Kabwe amshauri Job Ndugai
Bunge lataka tende zifutwe kodi mfungo wa Ramadhani
Mo Dewji afunguka jinsi anavyopiga pesa kupitia kilimo
RAIS wa Ufilipino, Rodrigo Duterte amesema hana mchezo katika vita dhidi ya dawa za kulevya na hata ikibainika mwanaye ni mmoja wa wahusika, hakuna namna, ni kumuua tu.
Rais huyo ametoa maelezo hayo baada ya kuwapo kwa tuhuma zinazomhusisha mmoja wa wanawe ambaye anachunguzwa na polisi. Paolo Duterte kijana mwenye umri wa miaka 42, ambaye pia ni mwanasiasa mwezi huu aliitwa mbele ya baraza la uchunguzi kuhojiwa na alikana tuhuma dhidi yake. Kijana huyo alituhumiwa na mmoja wa wanasiasa kwamba ni sehemu ya genge la raia wa China, akihusika kusaidia genge hilo katika usafirishaji wa dawa za kulevya kutoka China.
Lakini katika mazungumzo yake ya hivi karibuni Duterte hakulenga moja kwa moja kuzungumzia kwa kina tukio hilo linalomhusu mwanawe huyo lakini akaweka wazi kwamba, hakuna mwanawe anayejihusisha na dawa za kulevya lakini hata hivyo, ikibainika anapaswa kuadhibiwa kama wengine.
“Niliwahi kusema na kwa kweli amri yangu ni kwamba: kama ninao watoto wanaojihusisha na dawa za kulevya, wauawe tu kama wahalifu wengine ili kuondoa minong’ono ya watu,” alisema Duterte katika hotuba yake mbele ya watumishi wa serikali aliokutana nao katika Ikulu ya Manila.
“Kwa hiyo nakwambia wewe Pulong (hilo ni jina la utani la Paolo mwanawe anayetuhumiwa kwa dawa za kulevya), amri yangu inaelekeza uuawe kama itathibitika. Na nitamlinda polisi atakayekuua, kama itakuwa ni kweli,” alisema
Duterte mwenye umri wa miaka 72 sasa amekuwa akiendesha kampeni kali dhidi ya biashara ya dawa za kulevya nchini mwake na alikwishaagiza yeyote atakayebainika kujihusisha na biashara hiyo auwawe, iwe mtumiaji au mfanyabiasara wa dawa hizo.
Tangu aingie madarakani katikati ya mwaka jana, 2016, polisi wamekwishaua watu zaidi ya 3,800 katika operesheni ya kupambana na dawa za kulevya katika taifa hilo.
Duterte alikaririwa akisema “ninayo furaha kuua” watu milioni hata tatu hivi walioathiriwa kwa matumizi ya dawa za kulevya, na kama kuna watoto waliouawa kwenye operesheni dhidi ya dawa za kulevya basi ni ajali ya bahati mbaya tu.
Tayari wasaidizi kadhaa wa Duterte wamekuwa wakiwaonya waandishi wa habari kwamba wasitilie maanani kila anachokisema kiongozi huyo.
Post A Comment: