
Subscribe ndio neno gumu zaidi kwa wabongo kuliko kutafuna jiwe kama ilivyo kwa Waingereza kutamka Mwanjelwa..husema Monjela
Pamoja na vionjo hivyo..kwenye Simba Day ya mwaka huu ntakuja na style tofauti ya kutambulisha wachezaji...njoo ushuhudie mwenyew..usingoje kuhadithiwa ni Jtano hii pale dimba la Taifa... #SimbaDay #KibingwaZaidi 🇵🇪🇵🇪
Serikali yatoa tamko kuadimika mafuta ya kula nchini
Waziri Kigwangalla atetea ununuzi wa ndege
Zitto Kabwe amshauri Job Ndugai
Bunge lataka tende zifutwe kodi mfungo wa Ramadhani
Mo Dewji afunguka jinsi anavyopiga pesa kupitia kilimo
OPERESHENI endelevu ya Shirika la Umeme nchini (Tanesco), inayofanywa mkoani hapa, imewanasa baadhi ya wateja wakiiba umeme kwa zaidi ya siku 1000 bila malipo halali.
Udanganyifu huo unaofanywa kwenye nyumba za biashara na makazi kwa kutumia mita za Luku, umebaini baadhi ya wateja kujiunganishia umeme moja kwa moja na wengine kwa kuchezea mita.
Ukaguzi wa jana ulihusisha maeneo ya Ngaramtoni, Oldadai, Soko la Kilombero, Makao Mapya, Mjini Kati na King’ori wilayani Arumeru.
Ofisa Usalama Mwandamizi kutoka makao makuu ya Tanesco, Dar es Salaam, Lenin Kiobya, akiongoza kikosi maalumu cha ukaguzi, alisema, wizi huo unadhoofisha juhudi za kuletea maendeleo kwa wananchi hususan, katika kipindi hiki cha Tanzania ya viwanda.
Kikosi hicho kinahusisha Idara za Mawasiliano, Udhibiti wa Mapato, Usalama na maofisa wa Arusha.
Alisema wizi huo unalipunguzia shirika ufanisi wa kuhudumia wananchi kwa kukwepa kulipa malipo halali.
Alisema baadhi ya wafanyakazi ambao siyo waaminifu wanakula njama na wateja kuiba umeme.
Alisema katika eneo la King’ori operesheni hiyo ilifanikiwa kubaini baadhi ya wateja waliojiunganishia umeme, huku wengine wakifanya udanganyifu kwenye mita za Luku.
Alisema baadhi ya mita zimefungwa juu ya nguzo za barabarani, lakini kwa kutumia watu wanaoitwa ‘vishoka’ wanafanikiwa kuzichezea na hivyo kukwepa kulipa malipo halali.
Alisema kwa kutumia mifumo yao, wanaweza kuwabaini kwamba hawajanunua umeme wa Luku kwa muda mrefu.
“Tumefanya ukaguzi na kuwanasa wateja waliokwepa kununua umeme wa Luku kwa siku hadi 1,000 huku wakiendelea kupata umeme,” alisema.
Alisema ukaguzi wao una lengo la kukusanya na kudhibiti upotevu wa mapato ya shirika.
Kwa upande wake, Mdhibiti Mapato Tanesco mkoani hapa, Mhandisi Hassan Juma, aliwataka wafanyakazi wa shirika kushirikiana kuhakikisha mafundi wasio waaminifu wanaondoka.
Ukaguzi wa jana ulihusisha maeneo ya Ngaramtoni, Oldadai, Soko la Kilombero, Makao Mapya, Mjini Kati na King’ori wilayani Arumeru.
Ofisa Usalama Mwandamizi kutoka makao makuu ya Tanesco, Dar es Salaam, Lenin Kiobya, akiongoza kikosi maalumu cha ukaguzi, alisema, wizi huo unadhoofisha juhudi za kuletea maendeleo kwa wananchi hususan, katika kipindi hiki cha Tanzania ya viwanda.
Kikosi hicho kinahusisha Idara za Mawasiliano, Udhibiti wa Mapato, Usalama na maofisa wa Arusha.
Alisema wizi huo unalipunguzia shirika ufanisi wa kuhudumia wananchi kwa kukwepa kulipa malipo halali.
Alisema baadhi ya wafanyakazi ambao siyo waaminifu wanakula njama na wateja kuiba umeme.
Alisema katika eneo la King’ori operesheni hiyo ilifanikiwa kubaini baadhi ya wateja waliojiunganishia umeme, huku wengine wakifanya udanganyifu kwenye mita za Luku.
Alisema baadhi ya mita zimefungwa juu ya nguzo za barabarani, lakini kwa kutumia watu wanaoitwa ‘vishoka’ wanafanikiwa kuzichezea na hivyo kukwepa kulipa malipo halali.
Alisema kwa kutumia mifumo yao, wanaweza kuwabaini kwamba hawajanunua umeme wa Luku kwa muda mrefu.
“Tumefanya ukaguzi na kuwanasa wateja waliokwepa kununua umeme wa Luku kwa siku hadi 1,000 huku wakiendelea kupata umeme,” alisema.
Alisema ukaguzi wao una lengo la kukusanya na kudhibiti upotevu wa mapato ya shirika.
Kwa upande wake, Mdhibiti Mapato Tanesco mkoani hapa, Mhandisi Hassan Juma, aliwataka wafanyakazi wa shirika kushirikiana kuhakikisha mafundi wasio waaminifu wanaondoka.
Post A Comment: