
Subscribe ndio neno gumu zaidi kwa wabongo kuliko kutafuna jiwe kama ilivyo kwa Waingereza kutamka Mwanjelwa..husema Monjela
Pamoja na vionjo hivyo..kwenye Simba Day ya mwaka huu ntakuja na style tofauti ya kutambulisha wachezaji...njoo ushuhudie mwenyew..usingoje kuhadithiwa ni Jtano hii pale dimba la Taifa... #SimbaDay #KibingwaZaidi π΅πͺπ΅πͺ
Serikali yatoa tamko kuadimika mafuta ya kula nchini
Waziri Kigwangalla atetea ununuzi wa ndege
Zitto Kabwe amshauri Job Ndugai
Bunge lataka tende zifutwe kodi mfungo wa Ramadhani
Mo Dewji afunguka jinsi anavyopiga pesa kupitia kilimo
Rais mstaafu, Jakaya Kikwete amesema amefurahishwa namna Serikali ilivyojidhatiti kukarabati shule kongwe nchini ikiwamo Sekondari ya Kibaha, mkoani Pwani.
Kikwete alisema hayo juzi alipokuwa mgeni rasmi kwenye mahafali ya 50 ya kidato cha nne shuleni hapo, huku wanafunzi 116 wakihitimu katika michepuo ya sayansi, kilimo na biashara.
βKwa upande wa uhaba wa madarasa nitashirikiana na wadau wengine kuona namna ya kusaidia kutatua changamoto hiyo, kwa hadhi ya shule hii haipendezi kuwa na mrundikano wa wanafunzi darasani,β alisema Kikwete ambaye alisomea shule hiyo.
Akizungumza kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani, Mkuu wa Wilaya ya Kibaha, Assumpter Mshama alisema umefika wakati watu waliosoma katika shule hiyo kuangalia namna ya kuweka mipango madhubuti kusaidia kuboresha miundombinu.
Naye Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Shirika la Elimu Kibaha, Profesa Patrick Makungu alisema tangu shule hiyo ilipoanzishwa mwaka 1965, imeendelea kutoa wahitimu wa kidato cha nne na cha sita wengi wao waliendelea na masomo ya elimu ya juu na kurudi kuitumikia Serikali kwa kushika nafasi mbalimbali.
Post A Comment: