
Subscribe ndio neno gumu zaidi kwa wabongo kuliko kutafuna jiwe kama ilivyo kwa Waingereza kutamka Mwanjelwa..husema Monjela
Pamoja na vionjo hivyo..kwenye Simba Day ya mwaka huu ntakuja na style tofauti ya kutambulisha wachezaji...njoo ushuhudie mwenyew..usingoje kuhadithiwa ni Jtano hii pale dimba la Taifa... #SimbaDay #KibingwaZaidi π΅πͺπ΅πͺ
Serikali yatoa tamko kuadimika mafuta ya kula nchini
Waziri Kigwangalla atetea ununuzi wa ndege
Zitto Kabwe amshauri Job Ndugai
Bunge lataka tende zifutwe kodi mfungo wa Ramadhani
Mo Dewji afunguka jinsi anavyopiga pesa kupitia kilimo
Mbunge wa Kigoma Mjini kupitia chama cha ACT-Wazalendo Zitto Ruyagwa Kabwe ameungana na kauli iliyotolewa leo na Baraza la Vijana la CHADEMA kuitaka serikali kutia uzito uchunguzi wa jaribio la kuuliwa kwa Tundu Lissu na kuruhusu vyombo vya kimataifa.
Kwenye ukurasa wake wa twitter Zitto Kabwe amendika ujumbe akivitaka vyombo vingine vya kimataifa kufanya uchunguzi juu ya shambulio la Tundu Lissu, kwani haviamini vyombo vya ndani.
"Natafuta uchunguzi wa kujitegemea kimataifa juu ya jaribio la mauaji dhidi ya Mbunge Tundu Lissu, vyombo vya ndani sio vya kuviamini", aliandika Zitto Kabwe.
Zitto Kabwe aliendelea kwa kuandika kwamba watu waliofanya tukio hilo wana lengo la kuwafunga midomo wanapopaza sauti zao kupinga uonevu, hivyo hawatakiwi kukaa kimya kwani watakuwa wamewapa ushindi.
Jana asubuhi Baraza la Vijana CHADEMA limefanya mkutano na waandishi wa habari kuzungumzia tukio la kupigwa risasi kwa mbunge wa Singida Mashariki Tundu Antiphas Lissu, na kuitaka serikali itie uzito jambo hilo kwa kuunda tume huru maalum ya kuchuguza, pamoja na vyombo vya kimataifa.
Post A Comment: