
Subscribe ndio neno gumu zaidi kwa wabongo kuliko kutafuna jiwe kama ilivyo kwa Waingereza kutamka Mwanjelwa..husema Monjela
Pamoja na vionjo hivyo..kwenye Simba Day ya mwaka huu ntakuja na style tofauti ya kutambulisha wachezaji...njoo ushuhudie mwenyew..usingoje kuhadithiwa ni Jtano hii pale dimba la Taifa... #SimbaDay #KibingwaZaidi 🇵🇪🇵🇪
Serikali yatoa tamko kuadimika mafuta ya kula nchini
Waziri Kigwangalla atetea ununuzi wa ndege
Zitto Kabwe amshauri Job Ndugai
Bunge lataka tende zifutwe kodi mfungo wa Ramadhani
Mo Dewji afunguka jinsi anavyopiga pesa kupitia kilimo
Mamlaka ya Hali ya Hewa nchini (TMA) imesema mkoa wa Arusha unatarajiwa kuwa na mvua kubwa ambazo zitasababisha mafuriko katika baadhi ya maeneo.
Mvua hizo za vuli zinatarajiwa kuanza kunyesha Novemba 8 hadi Desemba 28 mwaka huu ambapo msimu wa vuli zinaonyesha kuwa mvua zitakuwa nyingi kuliko msimu uliopita.
Kwa mujibu wa taarifa kwa vyombo vya habari iliyotolewa na TMA ilisema mvua hizo zinatarajiwa kunyesha wastani hadi juu ya wastani katika maeneo ya Arusha Mjini na Vijijini, Karatu, Monduli na Ngorongoro.
Pia TMA ilisema kutakuwa na vipindi vya mvua kubwa vinavyotarajiwa kusababisha mafuriko na maji yanayopita kwa kasi hivyo wananchi na watumiaji wa pikipiki wanashauriwa kuchukua hatua.
Hatua stahiki zichukuliwe kukabiliana na ongezeko la unyevunyevu ardhini kwani inaweza kusababisha maporomoko ya ardhi yanayotokana na vipindi vifupi vya mvua hizo vinavyoweza kusababisha mafuriko.
“Wakulima wanashauriwa kuzalisha mazao ya chakula na biashara huku wafugaji watapata malisho ya mifugo na wanyamapor”, ilisema sehemui ya taarifa hiyo
Hata hivyo mvua za wastani hadi chini ya wastani zinatarajiwa kunyesha katika wilaya ya Meru na Mashariki mwa Longido hivyo wakulima wanashauriwa kupanda mazao yatakayokomaa kwa muda mfupi.
Kwa upande wa wafugaji wanashauriwa kuvuna, kuhifadhi malisho na maji kwa ajili ya matumizi kipindi cha ukame utakaoanzia Januari hadi Machi mwakani.
Taarifa hiyo ilisema vipindi vya upungufu wa unyevunyevu ardhini unatarajiwa kuathiri uzalishaji wa mazao ya kilimo na biashara pamoja na malisho ya mifugo na wanyamapori.
Hata hivyo taarifa hiyo ilisema ulinganifu wa mvua za vuli zinazotarajiwa kunyesha mwaka huu na msimu uliopita unaonyesha kuwa sawa na msimu uliopita.
Post A Comment: