
Subscribe ndio neno gumu zaidi kwa wabongo kuliko kutafuna jiwe kama ilivyo kwa Waingereza kutamka Mwanjelwa..husema Monjela
Pamoja na vionjo hivyo..kwenye Simba Day ya mwaka huu ntakuja na style tofauti ya kutambulisha wachezaji...njoo ushuhudie mwenyew..usingoje kuhadithiwa ni Jtano hii pale dimba la Taifa... #SimbaDay #KibingwaZaidi π΅πͺπ΅πͺ
Serikali yatoa tamko kuadimika mafuta ya kula nchini
Waziri Kigwangalla atetea ununuzi wa ndege
Zitto Kabwe amshauri Job Ndugai
Bunge lataka tende zifutwe kodi mfungo wa Ramadhani
Mo Dewji afunguka jinsi anavyopiga pesa kupitia kilimo
Mkuu wa Jeshi la Polisi mstaafu Omari Mahita amefunguka na kusema katika changamoto kubwa ambayo inalikbali jeshi la polisi Tanzania kwa sasa ni namna ya kudili na wanasiasa na kusema ni kazi kubwa kudili na wanasiasa.
Mahita alisema hayo juzi wakati alipokutana na Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini kwa sasa IGP Sirro na kusema licha ya changamoto hizo anaamini kuwa jeshi la polisi litasonga kutokana na mikakati ambayo wameweka katika kikao hicho kilichowakutanisha wakuu wa jeshi hilo wastaafu mbalimbali.
"Kuna changamoto nyingi lakini niwe muwazi tu changamoto ya kwanza ni namna ya kudili na wanasiasa, wanasiasa kudili nao ni kazi kubwa sana lakini nafikiri tutakwenda kutokana na mikakati ambayo tumeweka katika kikao hiki" alisema Mahita
Omari Mahita amewahi kuwa Mkuu wa jeshi la Polisi nchini Tanzania mnamo mwaka 1996 hadi mwaka 2006 ambapo alistaafu katika nafasi hiyo na kumuachia Saidi A. Mwema ambaye naye alihudumu kwa miaka nane kabla ya kijiti hicho kumuachia Ernest J. Mangu ambaye alihudumu kwa miaka minne kisha baadaye Rais Magufuli alimteua Simon Nyakoro Siro kuwa IGP wa Tanzania.
Post A Comment: