
Subscribe ndio neno gumu zaidi kwa wabongo kuliko kutafuna jiwe kama ilivyo kwa Waingereza kutamka Mwanjelwa..husema Monjela
Pamoja na vionjo hivyo..kwenye Simba Day ya mwaka huu ntakuja na style tofauti ya kutambulisha wachezaji...njoo ushuhudie mwenyew..usingoje kuhadithiwa ni Jtano hii pale dimba la Taifa... #SimbaDay #KibingwaZaidi 🇵🇪🇵🇪
Serikali yatoa tamko kuadimika mafuta ya kula nchini
Waziri Kigwangalla atetea ununuzi wa ndege
Zitto Kabwe amshauri Job Ndugai
Bunge lataka tende zifutwe kodi mfungo wa Ramadhani
Mo Dewji afunguka jinsi anavyopiga pesa kupitia kilimo
Idadi ya watu waliofariki kwa kuungua kwa moto nchini Ureno imeongezeka na kufikia 62.
Awali waliripotiwa watu 19, baadaye idadi hiyo iliongezeka na kufikia 25 ambayo mpaka sasa imefikia 62
Kwa mujibu wa maofisa wa serikali nchini humo, wengi walifariki walipokuwa wakiukimbia mji wa Pedrogao Grande, kilomita 50 kama (Maili 30) Kusini mashariki mwa Coimbra, kwa kutumia magari yao.
Maofisa wa Ureno wamesema kuwa, moto huo ulianza katika maeneo ya katikati mwa nchi hiyo na kusababisha vifo hivyo huku watu wengine wakijeruhiwa wakiwamo maafisa kadhaa wa zima moto.
Mpaka sasa chanzo kilichosababisha moto huo hakijabainika.
"Hili linaonekana ni janga baya zaidi ambalo tumewahi kushuhudia katika miaka ya hivi karibuni, katika moto wa nyika," amesema Waziri Mkuu wa nchi hiyo, Antonio Costa.
Waziri wa mambo ya ndani wa nchi hiyo João Gomes, amewaambia waandishi habari kuwa, watu 16 wameteketea ndani ya magari yao hadi kufa, wakati walipojaribu kukabiliana na moto huo mkubwa.
“Moto huo ulienea kwa kasi mno katika maeneo manne,” amesema Gomes.
Hispania imetuma ndege mbili zitakazosaidia kuuzima moto huo.
Post A Comment: