Malkia wa filamu , Wema Sepetu, Jumanne hii amepanda tena katika mahakama ya hakimu mkazi kisutu, Dar es salaam, kusikiliza kesi ya tuhuma za kutumia na kukutwa na madawa ya kulevya, ambapo upande wa Jamhuri umekamilisha upelelezi wa kesi inayomkabili msanii huyo.


Hakimu Mkazi Mkuu, Thomas Simba, ameahirisha kesi hiyo mpaka June 1, mwaka huu ambapo mahakama itasikiliza maelezo ya awali ya upelelezi huo.

Muigizaji huyo, ambaye yupo nje kwa dhamana baada kusota mahabusu kwa siku 7, anadaiwa kukutwa na msokoto wa bangi nyumbani kwake, kufuatia msako mkali wa kupambana na dawa za kulevya uliofanywa na ofisi ya mkoa wa Dar es salaam.
ads
Bonyeza HAPA kudownload applicationi ya SWAHILI NEWS kwenye simu yako ili kupata habari zetu Haraka
Share To:

SWAHIBA MEDIA STAFF

Habari , karibu katika mtandao wetu ili kuhabarika na stori zote za siku katika lugha yetu adhwim ya kiswahili, habarika wakati wote weka dunia kiganjani mwako na swahili news

Post A Comment: