
Subscribe ndio neno gumu zaidi kwa wabongo kuliko kutafuna jiwe kama ilivyo kwa Waingereza kutamka Mwanjelwa..husema Monjela
Pamoja na vionjo hivyo..kwenye Simba Day ya mwaka huu ntakuja na style tofauti ya kutambulisha wachezaji...njoo ushuhudie mwenyew..usingoje kuhadithiwa ni Jtano hii pale dimba la Taifa... #SimbaDay #KibingwaZaidi π΅πͺπ΅πͺ
Serikali yatoa tamko kuadimika mafuta ya kula nchini
Waziri Kigwangalla atetea ununuzi wa ndege
Zitto Kabwe amshauri Job Ndugai
Bunge lataka tende zifutwe kodi mfungo wa Ramadhani
Mo Dewji afunguka jinsi anavyopiga pesa kupitia kilimo
Msemaji wa Klabu ya Simba aliyefungiwa na TFF, Haji Manara amefunguka mengine mapya kwa kudai bado hajakubaliana na ubingwa wa ligi kuu Tanzania walioutwaa Yanga SC na kudai kuwa wao (Simba SC) ndiyo mabingwa wa ligi hiyo msimu huu.
Manara amebainisha hayo kupitia mitandao ya kijamii kwa kurusha vijembe kwa wapinzani wao wa jadi na kudai kwamba kama Serengeti Boys waliweza kushinda rufaa yao na kuweza kushiriki michuano ya vijana huko nchini Gabon basi nao watashinda bila shika.
"Wabongo bana kwa 'double standard' hawajambo, Serengeti Boys walikuwa Gabon kwa kushinda rufaa ila Simba hawastahili....Mjiandae kiakili Gongowazi, Simba ndiyo 'champion' msimu huu". Ameandika Manara
Tayari Simba imewasilisha malalamiko yao kwa Shirikisho la Soka la Kimataifa (FIFA) wakipinga kupokwa pointi 3 na TFF baada ya kupewa na bodi ya ligi kutokana na Kagera Sugar kumtumia mchezaji asiyestahili katika mechi dhidi yao, ambapo Kagera Sugar ilipata ushindi wa mabao 2-1.
Post A Comment: