Jukwaa la Wahariri nchini (TEF) limelaani kitendo cha waandishi wa habari kujeruhiwa katika tukio la uvamizi lililotokea katika mkutano wa CUF katika hotel ya Vina kata ya Mabibo ambapo waandishi wa habari walipigwa na kujeruhiwa


Katika taarifa hiyo ya (TEF) imemtaka Profesa Lipumba kujitokeza na kukiri na kuomba radhi kwa waandishi wa habari pamoja na Watanzania kufuatia tukio hilo kama alivyofanya Maalim Seif

"Tunamtaka Profesa Lipumba binafsi atoe kauli kuhusu tukio hili kama alivyofanya Maalim Seif ambaye binafsi aliandika barua rasmi kwa uongozi wa TEF akilaani kupigwa kwa waandishi wa habari na kutoa pole kwa wale waliomizwa na kupata mshtuko" Walisema viongozi wa TEF

Taarifa hiyo ya TEF ilikwenda mbali zaidi na kuwatahadharisha waandishi wa habari, wahariri kuwa wanapaswa kuwa makini pindi wanapokuwa wanaitwa na kundi hili la Lipumba kwa ajili ya kutoa habari zao 
ads
Bonyeza HAPA kudownload applicationi ya SWAHILI NEWS kwenye simu yako ili kupata habari zetu Haraka
Share To:

SWAHIBA MEDIA STAFF

Habari , karibu katika mtandao wetu ili kuhabarika na stori zote za siku katika lugha yetu adhwim ya kiswahili, habarika wakati wote weka dunia kiganjani mwako na swahili news

Post A Comment: