
Subscribe ndio neno gumu zaidi kwa wabongo kuliko kutafuna jiwe kama ilivyo kwa Waingereza kutamka Mwanjelwa..husema Monjela
Pamoja na vionjo hivyo..kwenye Simba Day ya mwaka huu ntakuja na style tofauti ya kutambulisha wachezaji...njoo ushuhudie mwenyew..usingoje kuhadithiwa ni Jtano hii pale dimba la Taifa... #SimbaDay #KibingwaZaidi π΅πͺπ΅πͺ
Serikali yatoa tamko kuadimika mafuta ya kula nchini
Waziri Kigwangalla atetea ununuzi wa ndege
Zitto Kabwe amshauri Job Ndugai
Bunge lataka tende zifutwe kodi mfungo wa Ramadhani
Mo Dewji afunguka jinsi anavyopiga pesa kupitia kilimo
OFISI ya Msajili wa Vyama ya Siasa imetoa orodha ya vyama vya siasa
vyenye usajili wa kudumu na viongozi wa vyama hivyo ambako inasisitiza
kuwa Profesa Ibrahim Lipumba ndiye Mwenyekiti wa Chama cha Wananchi
(CUF) na Katibu Mkuu ni Seif Shariff Hamad.
Kwa mujibu wa barua
hiyo ya Oktoba 4, 2016 iliyoandikwa kwenda kwa makatibu wakuu wa vyama
vyenye usajili wa kudumu, Profesa Lipumba ambaye Baraza Kuu la chama
hicho limetangaza kumfukuza uanachama, anaonekana kwenye orodha hiyo
kama Mwenyekiti wa CUF.
Jina la Profesa Lipumba ambaye alitangaza
kujiuzulu nafasi hiyo mwaka jana, limerejeshwa kwenye orodha na Msajili
wa Vyama ya Siasa baada ya yeye mwenyewe kutangaza kutengua barua yake
ya kujiuzulu.
Barua hiyo imevitaja vyama 22 ambayo vina usajili wa
kudumu na chama cha mwisho kusajiliwa ni Alliance for Change and
Transparency (ACT-Wazalendo) ambacho viongozi wake ni Anna Mghwira
ambaye ni Mwenyekiti na Katibu Mkuu ni Juma Sanani.
Chama hicho
kilipata usajili Mei 5, 2014. Vyama vingine ni Chama Cha Mapinduzi
ambacho Mwenyekiti wake ni John Magufuli na Katibu Mkuu ni Abdulrahman
Kinana. Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) Mwenyekiti wake ni
Freeman Mbowe na Katibu Mkuu ni Dk Vincent Mashinji.
Chama kingine
ni Union for Multiparty Democracy (UMD) ambacho Mwenyekiti wake ni
Kamana Masoud na Katibu Mkuu ni Moshi Kigundula. Chama cha National
Convention for Construction and Reform (NCCR-Mageuzi) Mwenyekiti wake ni
James Mbatia na nafasi ya katibu iko wazi.
DOWNLOAD
APP YETU YA SWAHIBA NEWS ILI UWEZE KUPATA HABARI ZOTE MOJA KWA MOJA
KUPITIA SIMU YAKO YA MKONONI BILA KUINGIA KWENYE WEBSITE,KUDOWNLOAD
BONYEZA HAPA
ANDIKA MAONI YAKO HAPO CHINI
Post A Comment: