OFISI ya Msajili wa Vyama ya Siasa imetoa orodha ya vyama vya siasa vyenye usajili wa kudumu na viongozi wa vyama hivyo ambako inasisitiza kuwa Profesa Ibrahim Lipumba ndiye Mwenyekiti wa Chama cha Wananchi (CUF) na Katibu Mkuu ni Seif Shariff Hamad.


Kwa mujibu wa barua hiyo ya Oktoba 4, 2016 iliyoandikwa kwenda kwa makatibu wakuu wa vyama vyenye usajili wa kudumu, Profesa Lipumba ambaye Baraza Kuu la chama hicho limetangaza kumfukuza uanachama, anaonekana kwenye orodha hiyo kama Mwenyekiti wa CUF.

Jina la Profesa Lipumba ambaye alitangaza kujiuzulu nafasi hiyo mwaka jana, limerejeshwa kwenye orodha na Msajili wa Vyama ya Siasa baada ya yeye mwenyewe kutangaza kutengua barua yake ya kujiuzulu.

Barua hiyo imevitaja vyama 22 ambayo vina usajili wa kudumu na chama cha mwisho kusajiliwa ni Alliance for Change and Transparency (ACT-Wazalendo) ambacho viongozi wake ni Anna Mghwira ambaye ni Mwenyekiti na Katibu Mkuu ni Juma Sanani.

Chama hicho kilipata usajili Mei 5, 2014. Vyama vingine ni Chama Cha Mapinduzi ambacho Mwenyekiti wake ni John Magufuli na Katibu Mkuu ni Abdulrahman Kinana. Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) Mwenyekiti wake ni Freeman Mbowe na Katibu Mkuu ni Dk Vincent Mashinji.

Chama kingine ni Union for Multiparty Democracy (UMD) ambacho Mwenyekiti wake ni Kamana Masoud na Katibu Mkuu ni Moshi Kigundula. Chama cha National Convention for Construction and Reform (NCCR-Mageuzi) Mwenyekiti wake ni James Mbatia na nafasi ya katibu iko wazi.

DOWNLOAD APP YETU YA SWAHIBA NEWS ILI UWEZE KUPATA HABARI ZOTE MOJA KWA MOJA KUPITIA SIMU YAKO YA MKONONI BILA KUINGIA KWENYE WEBSITE,KUDOWNLOAD BONYEZA HAPA  

ANDIKA MAONI YAKO HAPO CHINI
ads
Bonyeza HAPA kudownload applicationi ya SWAHILI NEWS kwenye simu yako ili kupata habari zetu Haraka
Share To:

SWAHIBA MEDIA STAFF

Habari , karibu katika mtandao wetu ili kuhabarika na stori zote za siku katika lugha yetu adhwim ya kiswahili, habarika wakati wote weka dunia kiganjani mwako na swahili news

Post A Comment: