Aliyekuwa mbunge wa Singida Kaskazini (CCM), Lazaro Nyalandu amewashukuru Watanzania waliompongeza na kuunga mkono uamuzi wake wa kujiondoa ndani ya chama hicho.
Pia, amesema si jambo la busara kuzushiana uongo.
Nyalandu ametumia akaunti zake za kijamii za Twitter, Facebook na Instagram kutoa kauli hizo siku mbili baada ya kutangaza uamuzi wa kujivua nafsi zote ndani ya CCM ikiwemo ubunge.
Pamoja na Nyalandu kueleza hayo amefunguka zaidi kwenye mahojiano maalum na Gazeti la Mwananchi ambayo yatachapishwa kesho Alhamisi



Post A Comment: