
Subscribe ndio neno gumu zaidi kwa wabongo kuliko kutafuna jiwe kama ilivyo kwa Waingereza kutamka Mwanjelwa..husema Monjela
Pamoja na vionjo hivyo..kwenye Simba Day ya mwaka huu ntakuja na style tofauti ya kutambulisha wachezaji...njoo ushuhudie mwenyew..usingoje kuhadithiwa ni Jtano hii pale dimba la Taifa... #SimbaDay #KibingwaZaidi π΅πͺπ΅πͺ
Serikali yatoa tamko kuadimika mafuta ya kula nchini
Waziri Kigwangalla atetea ununuzi wa ndege
Zitto Kabwe amshauri Job Ndugai
Bunge lataka tende zifutwe kodi mfungo wa Ramadhani
Mo Dewji afunguka jinsi anavyopiga pesa kupitia kilimo
Jeshi la Polisi mkoani Dodoma limekamata magari nane aina ya Nissan Patrol yenye rangi nyeupe na kuyafanyia ukaguzi kwa kushirikiana na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) kuhusiana na tukio la kusambuliwa kwa risasi Mbunge wa Singida mashariki Tundu Lissu .
Tukio hilo lilitokea Septemba 7 mwaka huu nyumbani kwake Area D Dodoma, wakati mbunge huyo akirejea nyumbani akitoka bungeni.
Taarifa hiyo imetolewa leo Septemba 9 na Kamanda wa Polisi mkoani Dodoma, Gilles Muroto, wakati akizungumza na waandishi wa habari mjini hapa.
"Uchunguzi wa awali umeonyesha kuwa wahalifu walikuwa na silaha ya SMG/SAR kutokana na maganda ya risasi yaliyokutwa eneo," amesema Muroto
Hata hivyo Kamanda Muroto amemtaka dereva wa Lissu, aliyemtaja kwa jina la Adam kujitokeza kituo cha Polisi ili aweze kutoa maelezo yake kuhusiana na tukio la kupigwa risasi kwani yeye ndiye alikuwa naye siku ya tukio.
Pia Kamanda Muroto amemtaka Katibu Mkuu wa Chadema Dk.Vicent Mashinji kufika Ofisi ya Mkuu wa Upelelezi Dodoma au Makao makuu ya upelelezi Dar es salaam ili kutoa ushahidi kuhusu tukio hilo.
Alifafanua kuwa Mashinji katika mkutano wake na waandishi wa habari alidai kuwa anawafahamu watu waliofanya shambulio hilo kwa hivyo amemtaka kutoa ushirikiano kwa jeshi la polisi .
Post A Comment: