
Subscribe ndio neno gumu zaidi kwa wabongo kuliko kutafuna jiwe kama ilivyo kwa Waingereza kutamka Mwanjelwa..husema Monjela
Pamoja na vionjo hivyo..kwenye Simba Day ya mwaka huu ntakuja na style tofauti ya kutambulisha wachezaji...njoo ushuhudie mwenyew..usingoje kuhadithiwa ni Jtano hii pale dimba la Taifa... #SimbaDay #KibingwaZaidi π΅πͺπ΅πͺ
Serikali yatoa tamko kuadimika mafuta ya kula nchini
Waziri Kigwangalla atetea ununuzi wa ndege
Zitto Kabwe amshauri Job Ndugai
Bunge lataka tende zifutwe kodi mfungo wa Ramadhani
Mo Dewji afunguka jinsi anavyopiga pesa kupitia kilimo
Katibu Mkuu wa CUF, Maalim Seif Sharif Hamad amewataka wanachama wa chama hicho kutokata tamaa wakiamini haki walioipata kupitia Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2015 itapatikana hivi karibuni.
Maalim Seif alisema hayo wakati akiwahutubia wanachama wa chama hicho katika mkutano mkuu wa Jimbo la Mtoni Wilaya ya Magharib A Unguja.
Seif alisema katika chama hicho wapo baadhi ya watu wamekuwa wakihisi kile anachokisema ni uongo.
Akizungumzia kuhusiana na kadhia inayoendelea kukikumba chama hicho alisema kwa sasa kila kitu kipo mahakamani na anaamini ndiyo chombo pekee cha kutoa haki kwa mujibu wa sheria.
Pia, Maalim Seif aliwahakikishia wanachama hao kuwa chama hicho kitaendelea kubaki salama licha ya misukosuko inayoendelea hivi sasa.
Awali, akifungua mkutano huo, Makamu Mwenyekiti Mstaafu Juma Duni Haji alisema CUF haipo tayari kuona damu inamwagika.
βChama hiki kitaendelea kubaki salama kama walivyokikuta wale wote wenye nia mbaya, watadhalilika na kuonekana na kila mtu kama wenzao,β alisema Haji.
Post A Comment: