
Subscribe ndio neno gumu zaidi kwa wabongo kuliko kutafuna jiwe kama ilivyo kwa Waingereza kutamka Mwanjelwa..husema Monjela
Pamoja na vionjo hivyo..kwenye Simba Day ya mwaka huu ntakuja na style tofauti ya kutambulisha wachezaji...njoo ushuhudie mwenyew..usingoje kuhadithiwa ni Jtano hii pale dimba la Taifa... #SimbaDay #KibingwaZaidi 🇵🇪🇵🇪
Serikali yatoa tamko kuadimika mafuta ya kula nchini
Waziri Kigwangalla atetea ununuzi wa ndege
Zitto Kabwe amshauri Job Ndugai
Bunge lataka tende zifutwe kodi mfungo wa Ramadhani
Mo Dewji afunguka jinsi anavyopiga pesa kupitia kilimo
Mara nyingi tumekuwa tukipokea maswali kuhusu maana ya kinga ya mwili wengi wakihitaji kujua kinga hizo ni kitu gani na zinaweza kuimarishwa vipi.
Kimsingi kinga za mwili huweza kupanda au kushuka kutokana na chakula unachokula au vinywaji unavyokunywa, lakini pia hata mazingira mazima ya maisha kwa ujumla
Mwili ulibuniwa na Mungu uweze kujitibu wenyewe bila kuhitaji dawa yoyote isipokuwa mwili unaweza kupambana na matatizo kutokana na vyakula unavyokula na kunywa. Shida ni kuwa watu wengi hatujuwi tule nini kwa ajili ya nini, mara nyingi tunakula ili tushibe.
Fanya chakula kiwe ndiyo dawa zako na si dawa kuwa chakula kwako. Kinga yako inapokuwa na nguvu ya kutosha huwezi kuugua ugonjwa wowote kirahisirahisi.
Vifuatavyo ni vyakula 14 vinavyoweza kukusaidia kuongeza kinga za mwili.
Matunda
Katika mlo wako wowote jitahidi usiache kujumuisha angalau tunda la aina moja. Kwa mujibu wa wataalamu wa afya, mtu asiyekula matunda ana hatari kubwa zaidi ya kupata magonjwa zaidi ya mlaji wa matunda.
Asali
Asali halisi husaidia kuimarisha pia kinga za mwili, lamba kijiko kimoja cha chakula kila siku kutwa mara tatu kwa mwezi mmoja itasaidia kuimarishakinga zako za mwili.
Juisi ya ubuyu
Pata kikombe kimoja cha juisi ya ubuyu kila siku kwani juisi hiyo inawingi wa vitami C nyingi ambazo husaidia pia kuimarisha kinga za mwili.
NaziMatumizi ya nazi huweza kusaidia kuimarisha kinga za mwili kutokana na kuwa na mafuta yaitwayo ‘medium chain fatty acids’ ambayo husaidia kuimarisha kinga ya mwili na hivyo kuupa mwili uwezo wa kuyashinda maradhi mbalimbali.
Tangawizi
Ni moja ya kiungo ambacho kinaingia kwenye orodha hii ya kuimarisha kinga za mwili pia.
Mtaalam Mandai anaeleza kuwa ukiona umeshindwa kabisa unaweza kuwasiliana naye ili akupatie moja ya kirutubisho murua ambacho huweza kusaidia kuongeza kinga za mwili (kipo hapo chini kwenye picha)
Post A Comment: