
Subscribe ndio neno gumu zaidi kwa wabongo kuliko kutafuna jiwe kama ilivyo kwa Waingereza kutamka Mwanjelwa..husema Monjela
Pamoja na vionjo hivyo..kwenye Simba Day ya mwaka huu ntakuja na style tofauti ya kutambulisha wachezaji...njoo ushuhudie mwenyew..usingoje kuhadithiwa ni Jtano hii pale dimba la Taifa... #SimbaDay #KibingwaZaidi 🇵🇪🇵🇪
Serikali yatoa tamko kuadimika mafuta ya kula nchini
Waziri Kigwangalla atetea ununuzi wa ndege
Zitto Kabwe amshauri Job Ndugai
Bunge lataka tende zifutwe kodi mfungo wa Ramadhani
Mo Dewji afunguka jinsi anavyopiga pesa kupitia kilimo
Fungamano la Makanisa ya Kilutheri Duniani (LWF) limekutana nchini kujadili namna ya kutetea watu waliotengwa wakiwemo wenye ulemavu.
Askofu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Dayosisi ya Mashariki na Pwani, Alex Malasusa ambaye ndiye mwenyeji wa ugeni huo amesema ipo haja ya kanisa kupaza sauti kuwatetea watu hao, wakiwemo wenye ulemavu, wanawake na watoto.
Dk Malasusa amesema kanisa lina wajibu wa kuona haki inatendeka kwa watu wote bila kubaguliwa hali zao na uwezo wao katika kufanya mambo.
Kuhusu sera zilizopo, Dk Malasusa amesema ifike wakati Serikali ianze kuziangalia kwa jicho la tatu ili kuhakikisha hakuna anayeachwa nyuma.
“Tumeona kuna kundi ambalo limeachwa nyuma kwa muda mrefu, mfano walemavu. Katika nchi nyingi za Kiafrika walemavu wamekuwa wakionekana kama laana, wanafungiwa ndani,” amesema.
Dk Malasusa amesema, “Katika nchi nyingi utamaduni wa watu ndiyo unawezesha utengenezaji wa sera, hivyo ifike wakati zitengenezwe sera ambazo zitawafanya watu wote wapate haki zao inavyostahili bila kujali ni mlemavu, mwanamke au mtoto.”
Akifungua kongamano hilo. Rais wa LWF na Askofu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Nigeria, Musa Filibus amesema haitoshi kwa kanisa kuilaumu au kuinyooshea kidole Serikali wakati lenyewe halijatimiza wajibu wake katika kukabiliana na changamoto zilizopo kwenye jamii.
Amesema wajibu huo unaanza kuonekana kwa kuonyesha njia mbadala za kukabiliana na changamoto hizo, ikiwa ni pamoja na kukemea vitendo visivyofaa.
“Tukiwaelimisha watoto wa kike tutapunguza mimba na ndoa za utotoni, vifo vinavyotokana na watoto kujifungua wakiwa na umri mdogo na mambo mengine kama hayo,” amesema.
Mshiriki wa kongamano hilo, Dk Hellen Kijo- Bisimba amesema ipo haja kwa kanisa kupambana na mifumo inayosababisha walemavu, wanawake na watoto kuendelea kuwa kwenye kundi maalumu.
“Kanisa limekuwa likiwasaidia kwa kuwapatia vyakula, mavazi, malazi na hata elimu watu wenye mahitaji maalumu lakini bado lilikuwa halijajielekeza kupambana na mifumo inayowasababishia hali hiyo. Tumeanza kugeukia huko na tunataka kukabiliana nayo ili tuwe na nguvu ya kupaza sauti kwa ngazi za juu zaidi,” amesema Dk Kijo –Bisimba.
Post A Comment: