Mwanaume mmoja aliyetajwa kwa jina la Timothy Johnson mwenye umri wa miaka 25, anashikiliwa na Jeshi la Polisi la Florida nchini Marekani kwa kosa la kumuua mpenzi wake Judith Therianos aliyekuwa na umri wa miaka 52, na kisha kuendelea kufanya naye mapenzi kwa muda.


Taarifa zilizotolewa na Mkuu wa kitengo cha polisi cha Florida, Chris Nocco zimeeleza kuwa tukio hilo lilitokea mwezi uliopita wakati wawili hao walipokuwa wanafanya mapenzi.

Nocco aliwaeleza waandishi wa habari kuwa uchunguzi wa polisi umebaini kuwa wakati wanaendelea kufanya mapenzi, mwanamke huyo alimtaka mtuhumiwa kutoendelea na ndipo alipomuua na kisha kuendelea na zoezi hilo kwa muda.

Kwa mujibu wa Polisi, Judith hakuonekana tangu Machi 14 mwaka huu kabla ya kubainika kuwa alikuwa ameuawa baada ya mwili wake kupatikana Aprili 7.
ads
Bonyeza HAPA kudownload applicationi ya SWAHILI NEWS kwenye simu yako ili kupata habari zetu Haraka
Share To:

SWAHIBA MEDIA STAFF

Habari , karibu katika mtandao wetu ili kuhabarika na stori zote za siku katika lugha yetu adhwim ya kiswahili, habarika wakati wote weka dunia kiganjani mwako na swahili news

Post A Comment: