ads

WAZIRI wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mwigulu Nchemba, ameshangazwa na kitendo cha wananchi kukimbia na kujifungia ndani vikundi vya kihalifu kama ‘panya road’ vinapofika kwenye mitaa yao.


Kutokana na hali hiyo, amesema anashangazwa kwa sababu vikundi hivyo vinaundwa na watoto wadogo wenye silaha za jadi ambazo wananchi wote wanazo, hivyo wanaweza kuwakabili.

Nchemba ambaye anasimamia jeshi la polisi lenye dhamana ya kulinda usalama wa raia na mali zao, alisema kitendo cha wananchi kukimbia vijana hao halikubaliki kwa kuwa polisi hawawezi kuwa kwenye kila mtaa kwa Wichita mmoja, hivyo ni lazima wananchi washiriki ulinzi.

“Haiwezekani mkasema ‘panya road’ wamekuja kwenye mtaa wapo wanne, watano au 10 halafu wakanyamazisha mtaa mzima. Hii haiwezekani chamber hawa wote wamekuja, wengine hawana hata silaha, wamekuja tu na vinanii hivi vya jadi (silaha) ambazo na sisi tunazo halafu wananyamazisha mtaa mzima. Hii sii lazima kusema tusubiri polisi, lazima tupambane kuhakikisha hatuachi wahalifu kutawala maeneo yetu.

DOWNLOAD APP YETU YA SWAHIBA NEWS ILI UWEZE KUPATA HABARI ZOTE MOJA KWA MOJA KUPITIA SIMU YAKO YA MKONONI BILA KUINGIA KWENYE WEBSITE,KUDOWNLOAD BONYEZA HAPA  

ANDIKA MAONI YAKO HAPO CHINI
ads
Bonyeza HAPA kudownload applicationi ya SWAHILI NEWS kwenye simu yako ili kupata habari zetu Haraka
Share To:

SWAHIBA MEDIA STAFF

Habari , karibu katika mtandao wetu ili kuhabarika na stori zote za siku katika lugha yetu adhwim ya kiswahili, habarika wakati wote weka dunia kiganjani mwako na swahili news

Post A Comment: