ads
KIKOSI CHA SAGRADA ESPERANCE

SIKU moja baada ya kutolewa na Al Ahly ya Misri katika hatua ya 16 Bora ya Ligi ya Mabingwa Afrika, Yanga imeangukia kwa Sagrada Esperanca ya Angola katika michuano ya kuwania ubingwa wa Kombe la Shirikisho Afrika.


Itakutana na Waangola hao katika hatua ya mtoano ambayo mshindi wake ataingia hatua ya makundi ya michuano hiyo inayoshika nafasi ya pili kwa ukubwa katika ngazi za klabu barani Afrika.

Kwa mujibu wa ratiba iliyopangwa na Shirikisho la Soka Afrika (CAF) jana alasiri, Yanga baada ya kufungwa 2-1 na Ahly juzi usiku huko Alexandria na hivyo kutolewa kwa jumla ya mabao 3-2, sasa itakipiga dhidi ya timu hiyo inayomilikiwa na Shirika la Madini la Taifa la Angola.

Itaanza kwa kuwakaribisha Waangola hao kati ya Mei 6 na 8 jijini Dar es Salaam na marudiano kuwa kati ya Mei 17 na 18 nchini Angola.

Haijafahamika Angola zitachuana katika mji gani, ingawa Sagrada iliyoanzishwa Desemba 22, mwaka 1976, yaani miaka 39 iliyopita, uwanja wake wa nyumbani upo Dundo, katika Jimbo la Lund Norte ambao una uwezo wa kuingiza mashabiki 3,000 kwa wakati mmoja.

Endapo itafanikiwa kuwang’oa Sagrada inayonolewa na Zoran Mackic, raia wa Serbia, Yanga itakuwa imejihakikishia kusaka mamilioni ya fedha katika michuano hiyo ambayo mshindi wake hutwaa kitita cha dola za Kimarekani 625,000 (Sh bilioni 1.36).

Mshindi wa pili hupata dola 432,000 (Sh milioni 907) wakati timu zinazoshika nafasi ya pili na ya tatu katika kila kundi hupata dola 239,000 (Sh milioni 500) na ya mwisho katika kundi, yaani inayoshika nafasi ya nne, huambulia dola 150,000 (Sh milioni 315).

DOWNLOAD APP YETU YA SWAHIBA NEWS ILI UWEZE KUPATA HABARI ZOTE MOJA KWA MOJA KUPITIA SIMU YAKO YA MKONONI BILA KUINGIA KWENYE WEBSITE,KUDOWNLOAD BONYEZA HAPA

ads
Bonyeza HAPA kudownload applicationi ya SWAHILI NEWS kwenye simu yako ili kupata habari zetu Haraka
Share To:

SWAHIBA MEDIA STAFF

Habari , karibu katika mtandao wetu ili kuhabarika na stori zote za siku katika lugha yetu adhwim ya kiswahili, habarika wakati wote weka dunia kiganjani mwako na swahili news

Post A Comment: