Serikali imesema kuwa baraza la uwezeshaji Wananchi(NEEC),limeanza
kutengeneza utaratibu wa namna ya fedha milioni 50 kwa kila kijiji
zitakavyoweza kuwafaisha wananchi wote vijijini wakiwemo Vijana na
Wanawake.
Akizungumza Bungeni Mjini Dodoma, Waziri wa nchini Sera, Uratibu na Bunge;
Kazi, Ajira, Vijana na Watu wenye Ulemavu, Jenista Muhagama, amesema
fedha hizo zitatolewa kwa kila Mtanzania bila kujali itikadi ya Vyama
kama habari ambazo zinasaambaa sasa kuwa watagawiwa wanachama wa CCM,
pekee.
Waziri Muhagama, amesema jambo hilo linalozungumzwa ni hofu tu ya baadhi ya watu na kuongeza kuwa serikali itazingatia utaratibu wa kisheria wa kuhakikisha fedha hizo zinawafikia Watanzania wote wanaohusika na mpanngo huo.
Mhe. Muhagama amesema kuwa fedha hizo zilikuwa ni ahadi ya rais wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli katika kampeni zake ambazo zipo katika ilani ya Chama cha Mapinduzi lakini haimaanishi kuwa fedha hizo zitagawiwa kwa wanachama wa chama hicho Pekee.
Waziri Muhagama, amesema jambo hilo linalozungumzwa ni hofu tu ya baadhi ya watu na kuongeza kuwa serikali itazingatia utaratibu wa kisheria wa kuhakikisha fedha hizo zinawafikia Watanzania wote wanaohusika na mpanngo huo.
Mhe. Muhagama amesema kuwa fedha hizo zilikuwa ni ahadi ya rais wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli katika kampeni zake ambazo zipo katika ilani ya Chama cha Mapinduzi lakini haimaanishi kuwa fedha hizo zitagawiwa kwa wanachama wa chama hicho Pekee.
DOWNLOAD
APP YETU YA SWAHIBA NEWS ILI UWEZE KUPATA HABARI ZOTE MOJA KWA MOJA
KUPITIA SIMU YAKO YA MKONONI BILA KUINGIA KWENYE WEBSITE,KUDOWNLOAD
BONYEZA HAPA
Post A Comment: