ads

MAKAMU wa Pili wa Rais wa Zanzibar, Balozi Seif Ali Iddi amesema Serikali italazimika kuchukuwa uamuzi mgumu katika kukabiliana na watu waliojenga nyumba bila ya vibali na bila uzingatiaji wa taratibu za ardhi.


Alisema uamuzi huo utahusu zaidi maeneo yaliyowekwa kwa ajili ya miradi ya kijamii, vianzio vya maji pamoja na mitaro ya kupitishia maji ya mvua.

Alitoa agizo hilo  kwa masheha wote wa wilaya mbili za Magharibi “A” na “ B” akiwataka kuanza kuorodhesha nyumba zote zilizojengwa bila ya kibali na katika maeneo yasiyostahiki.

“Tunakusudia kubomoa majengo yote yaliyojengwa bila ya kibali na kwenye maeneo ya njia za maji, ikiwa ni mwanzo wa uamuzi mgumu utakaochukuliwa na Serikali,” alisema Balozi Seif.

DOWNLOAD APP YETU YA SWAHIBA NEWS ILI UWEZE KUPATA HABARI ZOTE MOJA KWA MOJA KUPITIA SIMU YAKO YA MKONONI BILA KUINGIA KWENYE WEBSITE,KUDOWNLOAD BONYEZA HAPA
ads
Bonyeza HAPA kudownload applicationi ya SWAHILI NEWS kwenye simu yako ili kupata habari zetu Haraka
Share To:

SWAHIBA MEDIA STAFF

Habari , karibu katika mtandao wetu ili kuhabarika na stori zote za siku katika lugha yetu adhwim ya kiswahili, habarika wakati wote weka dunia kiganjani mwako na swahili news

Post A Comment: