ads

BAADA ya kuangukia katika michuano ya Kombe la Shirikisho ilikopangwa kukutana na Sagrada Esperanca ya Angola katika hatua ya mtoano, kocha wa Yanga, Hans van der Pluijm ameahidi makubwa.


Amesema anaamini timu yake ina nafasi kubwa ya kutinga hatua ya makundi, hivyo atafanya kila linalowezekana kuhakikisha dhamira yake inatimia, huku akitamba ana kikosi imara, isipokuwa kilikosa bahati mbele ya Al Ahly ya Misri, katikati ya wiki hii.

Usiku wa Jumatano iliyopita, Yanga ilitolewa kwa jumla ya mabao 3-2 na Al Ahly kwenye mchezo wa raundi ya pili wa Ligi ya Mabingwa Afrika, baada ya kukubali kipigo cha mabao 2-1, kwenye mchezo wa marudiano kwenye Uwanja wa Borg El Arab, jijini Alexandria, Misri.

Pluijm alisema matumaini hayo yanatokana na ari na ubora iliyokuwa nao kikosi chake ambacho kilipambana kufa kupona katika mchezo na Al Ahly, licha ya kutolewa kwenye michuano hiyo.

“Siwezi kuwadharau wapinzani wetu Esperanca, lakini naamini hawatakuwa bora kama ilivyokuwa kwa Al Ahly na kama hivyo, ndivyo basi kuna uwezekano mkubwa wa Yanga kucheza hatua ya makundi kwa sababu tupo kwenye kiwango bora hivi sasa,” alisema kocha huyo raia wa Uholanzi, lakini mwenye uzoefu mkubwa na soka ya Afrika.

Esperanca inayomilikiwa na Shirika la Taifa la Madini la Angola, ina nyota kadhaa akiwemo `babu’ mwenye umri wa miaka 37, lakini mwenye makali ya upachikaji mabao, Arsenio Sebastiao Cabungula maarufu kama Love ambaye mwaka 2006 alikuwa miongoni mwa nyota wa Angola waliocheza Kombe la Dunia nchini Ujerumani.
DOWNLOAD APP YETU YA SWAHIBA NEWS ILI UWEZE KUPATA HABARI ZOTE MOJA KWA MOJA KUPITIA SIMU YAKO YA MKONONI BILA KUINGIA KWENYE WEBSITE,KUDOWNLOAD BONYEZA HAPA

ads
Bonyeza HAPA kudownload applicationi ya SWAHILI NEWS kwenye simu yako ili kupata habari zetu Haraka
Share To:

SWAHIBA MEDIA STAFF

Habari , karibu katika mtandao wetu ili kuhabarika na stori zote za siku katika lugha yetu adhwim ya kiswahili, habarika wakati wote weka dunia kiganjani mwako na swahili news

Post A Comment: