ads

Profesa Ibrahim Lipumba ameunda kamati ya maadili na nidhamu kwa ajili ya kuwahoji wanachama watovu wa nidhamu, katika siku ambayo Wakala wa Usajili, Ufilisi na Udhamini (Rita) umeeleza sababu za kuitambua bodi ya wadhamini ya msomi huyo.


Profesa Lipumba anatambuliwa na Msajili wa Vyama vya Siasa kuwa mwenyekiti wa CUF, lakini anapingwa vikali na upande unaoongozwa na katibu mkuu, Maalim Seif Sharif Hamad ambao unasema alishajiuzulu uenyekiti na Mkutano Mkuu kuridhia.

Jana ofisa mtendaji mkuu wa Rita, Emmy Hudson aliiambia Mwananchi kuwa aliisajili bodi hiyo mpya baada ya kupata uthibitisho wa Msajili wa Vyama vya Siasa kuwa upande wa Profesa Lipumba ndio unaotambulika na ofisi yake.

Hudson alisema kwa kifupi kuwa walipokea maombi ya kusajili bodi ya wadhamini Machi 23 kutoka pande zote mbili, lakini hawakuyafanyia kazi siku hiyo.

Alisema walianza kushughulikia maombi hayo taratibu na baadaye kuomba uthibitisho kwa Msajili kuhusu upande ambao unatambulika.

“Baada ya kuzungumza na pande zote mbili, baadaye msajili alisema anautambua upande wa Lipumba. Tulifuatilia taarifa kwa msajili kwa kuwa ndiye mwenye dhamana. Sisi sote turudi kwa msajili atuambie kwa nini anamtambua Lipumba na siyo Maalim,” alisema Hudson.

Juni 22, CUF upande wa Profesa Lipumba uliitambulisha rasmi bodi mpya ya wadhamini wakidai kuwa imesajiliwa na Rita Juni 12. Pia, walieleza kuwa kusajiliwa kwa bodi hiyo kunaifanya CUF iwe moja na kuondoa migogoro yote iliyoigawa.

Credit - Mwananchi
ads
Bonyeza HAPA kudownload applicationi ya SWAHILI NEWS kwenye simu yako ili kupata habari zetu Haraka
Share To:

SWAHIBA MEDIA STAFF

Habari , karibu katika mtandao wetu ili kuhabarika na stori zote za siku katika lugha yetu adhwim ya kiswahili, habarika wakati wote weka dunia kiganjani mwako na swahili news

Post A Comment: