ads

Wachezaji saba walikosekana wakati kocha mpya wa Yanga, George Lwandamina akishudia kwa mara ya kwanza mazoezi ya timu hiyo yaliyofanyika jana asubuhi kwenye Uwanja wa Chuo cha Polisi, Kurasini, Dar es Salaam.


Katika mazoezi hayo ya jana yaliyodumu kwa saa mbili, wachezaji waliokosa ni kipa, Benno Kakolanya, mabeki Hassan Kessy, Vincent Bossou, kiungo Haruna Niyonzima na washambuliaji Donald Ngoma, Malimi Busungu na Obrey Chirwa.

Hata hivyo, Katibu Mkuu wa Yanga, Baraka Deusdedit alisema kuwa wachezaji ambao hawakuonekana mazoezini, wana ruhusa maalumu ya uongozi.

Mabingwa hao watetezi wa Ligi Kuu wameanza mazoezi kujiandaa na mzunguko wa pili wa Ligi Kuu utakaoanza Desemba 17. Yanga itaanza raundi ya pili kwa kupambana na JKT Ruvu.

Katika mazoezi hayo, Lwandamina alikuwa nje na mkurugenzi mpya wa ufundi wa Yanga, Hans Pluijm na kumwachia jukumu kocha msaidizi, Juma Mwambusi kuwanoa wachezaji.

Lwandamina alionekana akiandika vitu mbalimbali katika kile alichokuwa akikiona katika mazoezi hayo na baada ya mazoezi aliliambia gazeti hili kuwa kazi yake kubwa katika mazoezi hayo ya kwanza ni kufuatilia ubora wa wachezaji wake.
“Nilikuwa ninaangalia ubora wa wachezaji, lakini kazi rasmi nitaanza kesho (leo) na nimeridhishwa na ubora wa wachezaji nafikiri kidogo nimeanza kupata mwanga wa wapi pa kuanzia,” alisema Lwandamina.
DOWNLOAD APP YETU YA SWAHIBA NEWS ILI UWEZE KUPATA HABARI ZOTE MOJA KWA MOJA KUPITIA SIMU YAKO YA MKONONI BILA KUINGIA KWENYE WEBSITE,KUDOWNLOAD BONYEZA HAPA  

ANDIKA MAONI YAKO HAPO CHINI
ads
Bonyeza HAPA kudownload applicationi ya SWAHILI NEWS kwenye simu yako ili kupata habari zetu Haraka
Share To:

SWAHIBA MEDIA STAFF

Habari , karibu katika mtandao wetu ili kuhabarika na stori zote za siku katika lugha yetu adhwim ya kiswahili, habarika wakati wote weka dunia kiganjani mwako na swahili news

Post A Comment: