ads

SIKU moja baada ya kuanza kibarua chake kipya cha kuinoa klabu ya Yanga, kocha mpya wa mabingwa hao wa soka nchini, George Lwandamina ameonesha kutoridhishwa na ubora wa uwanja unaotumiwa kwa mazoezi wa Chuo cha Polisi Kurasini na kuutaka uongozi kutafuta uwanja mwingine.


Mzambia huyo alianza rasmi kibarua chake Jumatatu, ambapo baada ya kumalizika kwa mazoezi yaliyohudhuriwa na wachezaji 18, aliuomba uongozi kumuonesha viwanja vingine vitatu tofauti ili kuchagua ulio bora tofauti na huo wa Polisi Kurasini.

Lwandamina alisema uwanja huo siyo bora kutokana na mfumo wa soka anaotaka kuwafundisha wachezaji wake, hivyo atafurahi kama uongozi utafanya jitihada za kupata uwanja mwingine ambao utakuwa muafaka kwa kile anachotaka kuwafundisha vijana wake.

“Uwanja huu ni mzuri kwa utulivu, lakini una mapungufu mengi ikiwemo sehemu ya kuchezea kukosa usawa, jambo ambalo linasababisha mpira kudunda dunda na kumpa tabu mchezaji kuumiliki,”alisema Lwandamina.

Kocha huyo alisema anaamini Tanzania kuna viwanja vingi vizuri ukiacha ule wa Taifa, ambao umefungiwa kwa sasa kwa timu hizo za Simba na Yanga, hivyo viongozi watapambana ili kuwatafutia uwanja mzuri ambao utamwezesha yeye na wasaidizi wake kutoa mafunzo mazuri kwa wachezaji wao.

Akilizungumzia hilo, Meneja wa timu hiyo, Hafidh Salehe alisema watalifanyia kazi ombi la kocha huyo na muda si mrefu watalipatia ufumbuzi ili timu hiyo ihamishie mazoezi yake kwa ajili ya kujiandaa na mzunguko wa pili wa Ligi Kuu na michuano ya kimataifa.

Siku za nyuma Yanga ilikuwa ikipendelea kufanya mazoezi yake kwenye viwanja vitatu ule wa Uhuru, Gymkhana au Boko Veterani na kutokana na maombi ya Lwandamina pengine uongozi ukapendekeza timu kufanya mazoezi yake moja kati ya viwanja hivyo.

Hata hivyo, Tanzania imekuwa na matatizo makubwa ya viwanja huku klabu kongwe za Yanga na Simba zikiwa hazina viwanja vyao na kubaki kukodisha.
DOWNLOAD APP YETU YA SWAHIBA NEWS ILI UWEZE KUPATA HABARI ZOTE MOJA KWA MOJA KUPITIA SIMU YAKO YA MKONONI BILA KUINGIA KWENYE WEBSITE,KUDOWNLOAD BONYEZA HAPA  

ANDIKA MAONI YAKO HAPO CHINI
ads
Bonyeza HAPA kudownload applicationi ya SWAHILI NEWS kwenye simu yako ili kupata habari zetu Haraka
Share To:

SWAHIBA MEDIA STAFF

Habari , karibu katika mtandao wetu ili kuhabarika na stori zote za siku katika lugha yetu adhwim ya kiswahili, habarika wakati wote weka dunia kiganjani mwako na swahili news

Post A Comment: