![ads](http://1.bp.blogspot.com/-J5aEnGVep5k/WJTrf2fzuPI/AAAAAAAAU5U/_iuE-DY1RHAM5_hqPHb-UuNbabG2xn2nwCK4B/s1600/AdvertiseHere.jpg)
Siku moja baada ya Mchungaji wa Kanisa la Maombezi, Anthony Lusekelo
kudaiwa kumfanyia fujo jirani yake, mchungaji huyo maarufu kwa jina la
Mzee wa Upako ameibuka kanisani kwake na kusema msemo wake wa kawaida
kuwa, ‘watashindana lakini hawatashinda.’
Pia alisema kuwa alitaka kusema jambo, lakini hatazungumza kama wengi walivyodhani.
Lusekelo
aliyasema hayo jana jioni katika ibada ya Ijumaa kanisani kwake, Ubungo
Kibangu '
“Nimeyaona
magazeti hapa, ooh Mzee wa Upako, ooh Mzee wa Upako, sisemi. Sasa leo
yupo hapa, na kwa taarifa yao watashindana sana, lakini hawatashinda.
Hii ni kama kumpiga chura teke,” alisema huku akishangiliwa na waumini
wake.
Kabla ya kuzungumza, Lusekelo aliingia kanisani akiimba wimbo wa kuabudu ‘Niguse Tena’ huku waumini wote wakiwa wamesimama.
Akiwa
amevalia shati jeupe la kitenge na suruali nyeusi huku kanisa likiwa
limezingirwa na walinzi kila kona, mchungaji huyo aliingia na kusimama
madhabahuni kisha kuwasalimu waumini: “Nawasalimu katika jina la Bwana.”
Baada ya
salamu hiyo, alianza kuimba wimbo mwingine na waumini hao wakaanza
kuimba pamoja naye huku wakipita mmoja mmoja mbele kumtuza fedha.
Wimbo ulipoisha, waumini waliketi na Lusekelo alianza kuhubiri kwa kufungua Biblia katika kitabu cha 2 Timotheo 4.
Katikati
ya mahubiri hayo, alidokeza na kusema kuna watu walikuwa wanasubiri
kuona Mzee wa Upako hayupo na wanataka aseme, lakini hatasema chochote.
“Kuna
kitu nilikuwa nataka nikiseme, lakini sitakisema ili waendelee kusema
haohao waliokuwa wanasema. Sisemi chochote. Hao waliosema wakawaulize
wenyewe,” alisema bila kufafanua zaidi.
Ingawa alisema hatasema chochote, mahubiri yake yalionekana kama kujibu mapigo.
“Imani
yangu ndiyo ilikuwa mwisho, kwa sababu maadui watakuwa wengi lakini
watajikuta wanapiga risasi kule, kumbe adui yupo huku… vita ni kutulia,”
alisema.
“Adui
yako hataacha kuwa adui yako. Jiepushe sana na watu hao. Lakini mimi
ninaamini Mungu atawalipa sawa na amri yake wakati ukifika.”
Aliendelea na kusema wanadamu wamekengeuka na kuziacha njia za uzima na kuzigeukia njia zao wenyewe.
“Wakati
wote watu watakataa kusikia ule ukweli, Ogopa sana anayekataa
kukusikiliza, watakapozigeukia njia zao wenyewe, wakiacha kusikia
ukweli, jua kuna tatizo, akiacha kukusikiliza ni hatari sana jua kuna
rushwa. Ukiona anaacha kukusikiliza kaa tayari” alisema.
Mchungaji huyo aliendelea kuhubiri na kusema ni marufuku kumuhuku
mu mtu kabla ya kumsikiliza.
“Hao
ndiyo marafiki wanafiki.Nao wakajiepusha wasisikie yaliyo kweli na
watageukia hadithi za uongo. Uongo ukisemwa sana hubadilika na kuwa ni
kweli.
“Wale
wazee wa Israel walitunga uongo, na wakatoa fedha uongo usambazwe, ule
uongo mpaka leo bado unaitafuna Israel.” alisema Mzee wa Upako.
DOWNLOAD
APP YETU YA SWAHIBA NEWS ILI UWEZE KUPATA HABARI ZOTE MOJA KWA MOJA
KUPITIA SIMU YAKO YA MKONONI BILA KUINGIA KWENYE WEBSITE,KUDOWNLOAD
BONYEZA HAPA
ANDIKA MAONI YAKO HAPO CHINI
Post A Comment: