ads

 Siku moja baada ya Mchungaji wa Kanisa la Maombezi, Anthony Lusekelo kudaiwa kumfanyia fujo jirani yake, mchungaji huyo maarufu kwa jina la Mzee wa Upako ameibuka kanisani kwake na kusema msemo wake wa kawaida kuwa, ‘watashindana lakini hawatashinda.’


Pia alisema kuwa alitaka kusema jambo, lakini hatazungumza kama wengi walivyodhani.

Lusekelo aliyasema hayo jana jioni katika ibada ya Ijumaa kanisani kwake, Ubungo Kibangu '

“Nimeyaona magazeti hapa, ooh Mzee wa Upako, ooh Mzee wa Upako, sisemi. Sasa leo yupo hapa, na kwa taarifa yao watashindana sana, lakini hawatashinda. Hii ni kama kumpiga chura teke,” alisema huku akishangiliwa na waumini wake.

Kabla ya kuzungumza, Lusekelo aliingia kanisani akiimba wimbo wa kuabudu ‘Niguse Tena’ huku waumini wote wakiwa wamesimama.

Akiwa amevalia shati jeupe la kitenge na suruali nyeusi huku kanisa likiwa limezingirwa na walinzi kila kona, mchungaji huyo aliingia na kusimama madhabahuni kisha kuwasalimu waumini: “Nawasalimu katika jina la Bwana.”
Baada ya salamu hiyo, alianza kuimba wimbo mwingine na waumini hao wakaanza kuimba pamoja naye huku wakipita mmoja mmoja mbele kumtuza fedha.

Wimbo ulipoisha, waumini waliketi na Lusekelo alianza kuhubiri kwa kufungua Biblia katika kitabu cha 2 Timotheo 4.

Katikati ya mahubiri hayo, alidokeza na kusema kuna watu walikuwa wanasubiri kuona Mzee wa Upako hayupo na wanataka aseme, lakini hatasema chochote.

“Kuna kitu nilikuwa nataka nikiseme, lakini sitakisema ili waendelee kusema haohao waliokuwa wanasema. Sisemi chochote. Hao waliosema wakawaulize wenyewe,” alisema bila kufafanua zaidi.

Ingawa alisema hatasema chochote, mahubiri yake yalionekana kama kujibu mapigo.

“Imani yangu ndiyo ilikuwa mwisho, kwa sababu maadui watakuwa wengi lakini watajikuta wanapiga risasi kule, kumbe adui yupo huku… vita ni kutulia,” alisema.

“Adui yako hataacha kuwa adui yako. Jiepushe sana na watu hao. Lakini mimi ninaamini Mungu atawalipa sawa na amri yake wakati ukifika.”

Aliendelea na kusema wanadamu wamekengeuka na kuziacha njia za uzima na kuzigeukia njia zao wenyewe.

“Wakati wote watu watakataa kusikia ule ukweli, Ogopa sana anayekataa kukusikiliza, watakapozigeukia njia zao wenyewe, wakiacha kusikia ukweli, jua kuna tatizo, akiacha kukusikiliza ni hatari sana jua kuna rushwa. Ukiona anaacha kukusikiliza kaa tayari” alisema.

Mchungaji huyo aliendelea kuhubiri na kusema ni marufuku kumuhuku
mu mtu kabla ya kumsikiliza.

“Hao ndiyo marafiki wanafiki.Nao wakajiepusha wasisikie yaliyo kweli na watageukia hadithi za uongo. Uongo ukisemwa sana hubadilika na kuwa ni kweli.

“Wale wazee wa Israel walitunga uongo, na wakatoa fedha uongo usambazwe, ule uongo mpaka leo bado unaitafuna Israel.” alisema Mzee wa Upako.

DOWNLOAD APP YETU YA SWAHIBA NEWS ILI UWEZE KUPATA HABARI ZOTE MOJA KWA MOJA KUPITIA SIMU YAKO YA MKONONI BILA KUINGIA KWENYE WEBSITE,KUDOWNLOAD BONYEZA HAPA  

ANDIKA MAONI YAKO HAPO CHINI
ads
Bonyeza HAPA kudownload applicationi ya SWAHILI NEWS kwenye simu yako ili kupata habari zetu Haraka
Share To:

SWAHIBA MEDIA STAFF

Habari , karibu katika mtandao wetu ili kuhabarika na stori zote za siku katika lugha yetu adhwim ya kiswahili, habarika wakati wote weka dunia kiganjani mwako na swahili news

Post A Comment: