ads

Polisi katika mji wa Bangalore kusini mwa India wanamsaka dereva mwenye gari ambalo hutumiwa kusafirisha pesa za kuwekwa kwenye mitambo ya ATM baada yake kutoweka na rupee milioni 9.2 ($134,000; £107,000) zikiwa kwa noti mpya za rupee elfu 2.


Dominic Selvaraj, anadaiwa kutoweka na gari hilo pale mwenzake alipoingia ndani ya choo cha benki kuenda haja.

Polisi wamesema gari hilo lilipatika limeegeshwa mjini Bangalore baadaye siku hiyo.

Mashine za ATM zimeshuhudia milolongo mirefu wa watu tangu noti za 500 na 1000 kupigwa marufuku kama njia ya kukabiliana na ufisadi.

Serikali imezindua noti mpya za rupee 500 na 2,000, lakini bado hazijaanza kuzunguka vyema kwenye mfumo wa pesa nchini humo na benki nyingi zinakabiliwa na uhaba wa pesa hizo mpya.

Afisa mkuu wa polisi Charan Reddy amemwambia mwandishi wa BBC Imran Qureshi kwamba Bw Selvaraj alikuwa ameajiriwa kama dereva wiki tatu zilizopita na kampuni ya usafirishaji wa pesa kutoka kwenye benki hadi mitambo ya ATM.

DOWNLOAD APP YETU YA SWAHIBA NEWS ILI UWEZE KUPATA HABARI ZOTE MOJA KWA MOJA KUPITIA SIMU YAKO YA MKONONI BILA KUINGIA KWENYE WEBSITE,KUDOWNLOAD BONYEZA HAPA  

ANDIKA MAONI YAKO HAPO CHINI
ads
Bonyeza HAPA kudownload applicationi ya SWAHILI NEWS kwenye simu yako ili kupata habari zetu Haraka
Share To:

SWAHIBA MEDIA STAFF

Habari , karibu katika mtandao wetu ili kuhabarika na stori zote za siku katika lugha yetu adhwim ya kiswahili, habarika wakati wote weka dunia kiganjani mwako na swahili news

Post A Comment: