ads

RAIS mstaafu wa awamu ya tatu ambaye pia ni Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM), Benjamini Mkapa, amewataka viongozi wa vyuo vikuu nchi nzima kukutana kwa lengo la kujadili gharama za uendeshaji wa vyuo hivyo nchini.


Ametoa kauli hiyo wakati wa mahafali ya saba ya chuo hicho na kufafanua, “Jambo hilo lisipozungumzwa sasa linaweza kuwa tatizo kubwa siku za usoni”.

Amesema nchi bado changa lakini kwa sababu uchumi wa nchi ni mchanga kwa maana hiyo bado ni nchi masikini, hivyo wanajitahidi kukuza uchumi kwa kasi lakini matarajio na idadi ya wanachuo na wanafunzi ni kubwa na inazidi kukua siku hadi siku.

Amesema kukua huko ni lazima kufanane na uwezeshaji wa vyuo vyote kutoa elimu na kama bajeti hazitoshelezi yatapatikana matokeo hafifu na ushindani katika jumuiya ya Afrika Mashariki, Afrika na dunia nzima na kwa wahitimu hapa nchini utakuwa mgumu sana.

Mkapa amesema amri na maagizo peke yake hayatatui tatizo ila viongozi wakikaa pamoja wanaweza kujadili mikakati ya kugharamia jambo ambalo linanza kuimarisha ubora wa elimu na umakini wa rasilimali watu wanaotokana na vyuo vikuu vya serikali.

Amesema chuo cha UDOM kutegemea uwekezaji wakati chenyewe kinawekezwa ni kujidanganya, hivyo wakiamua kufanya mkutano wanaweza kupata ufumbuzi katika vyuo hivyo.

Mwenyekiti wa chuo kikuu cha UDOM, Gaudencia Kabaka katika risala yake alisema changamoto kubwa waliyonayo chuoni hapo ni kutolipwa kwa wakati fedha za ada na bodi ya mikopo.

Ameisema kuwa mwaka 2015/2016 ada ya Sh bilioni 6.5 ambazo zilitakiwa kulipwa na bodi ya mikopo hazijalipwa mpaka sasa. Jumla ya wanafunzi 4,839 walihitibu,kati ya wahitimu hao waliopata cheti ni 394, stashahada 4,046, shahada ya kwanza 242, stastahada za juu 62 na shahada za uzamili na 17 shahada za uzamivu.

DOWNLOAD APP YETU YA SWAHIBA NEWS ILI UWEZE KUPATA HABARI ZOTE MOJA KWA MOJA KUPITIA SIMU YAKO YA MKONONI BILA KUINGIA KWENYE WEBSITE,KUDOWNLOAD BONYEZA HAPA  

ANDIKA MAONI YAKO HAPO CHINI
ads
Bonyeza HAPA kudownload applicationi ya SWAHILI NEWS kwenye simu yako ili kupata habari zetu Haraka
Share To:

SWAHIBA MEDIA STAFF

Habari , karibu katika mtandao wetu ili kuhabarika na stori zote za siku katika lugha yetu adhwim ya kiswahili, habarika wakati wote weka dunia kiganjani mwako na swahili news

Post A Comment: