ads
MBUNGE wa Ukonga, Mwita Waitara (Chadema), alikamatwa na polisi jijini Dar es Salaam akituhumiwa kuingilia utekelezaji wa majukumu ya jeshi hilo jana.


Waitara alikamatwa eneo la Uvikiuta alipokuwa akifuatilia mgogoro wa muda mrefu wa ardhi na kupelekwa kwenye Kituo cha Polisi Chang'ombe, Temeke jijini.

 Waitara alidai hakuzuia jeshi hilo kutekeleza majukumu yake isipokuwa alihoji sababu za nyumba za wananchi wa Mtaa wa Uvikiuta uliopo Kata ya Ukonga kuvunjwa pasi na taarifa, na kampuni moja ya udalali chini ya jeshi hilo.

Alisema jana majira ya saa mbili asubuhi alipata taarifa za wananchi wake kuvamiwa na watu wanaojita kampuni ya madalali ambao walifika katika eneo lao na kuanza kuvunja nyumba na alipoamua kuhoji sababu za zoezi hilo kufanywa bila taarifa, alikamtwa na kupelekwa polisi kwa madai kwamba amezuia jeshi kutekeleza majukumu yao.

“Mimi sijazuia jeshi kufanya kazi yake, nilikuwa nahoji tu kwa nini iweje ghafla hivyo na ninavyofahamu mgogoro huo ulikuwa wa siku nyingi na kesi yake bado iko mahakamani," alisema Waitara. "Sasa kwa nini waje kuvunja wakati kesi inaendelea na hata hivyo wananchi hawajapewa taarifa?”

Alisema kuwa jana mchana alipewa fomu ya kuandika maelezo yake, lakini akaomba a
siandike chochote mpaka awasiliane na Mwanasheria wake.

“Tangu saa nne asubuhi nilikuwa nahojiwa polisi hadi saa 12 jioni ndiyo nimetolewa. Wanadai nimezuia polisi kutekeleza majukumu yao, wamekubali kuniachia kwa dhamana lakini wameniambia niende kesho saa mbili asubuhi kwa RCO," alisema Waitara jana.
DOWNLOAD APP YETU YA SWAHIBA NEWS ILI UWEZE KUPATA HABARI ZOTE MOJA KWA MOJA KUPITIA SIMU YAKO YA MKONONI BILA KUINGIA KWENYE WEBSITE,KUDOWNLOAD BONYEZA HAPA  

ANDIKA MAONI YAKO HAPO CHINI
ads
Bonyeza HAPA kudownload applicationi ya SWAHILI NEWS kwenye simu yako ili kupata habari zetu Haraka
Share To:

SWAHIBA MEDIA STAFF

Habari , karibu katika mtandao wetu ili kuhabarika na stori zote za siku katika lugha yetu adhwim ya kiswahili, habarika wakati wote weka dunia kiganjani mwako na swahili news

Post A Comment: