ads

Katibu wa chama cha wananchi CUF, Maalim Seif amelishutumu jeshi la polisi kwa kile alichodai kuvuruga mikutano inayoandaliwa na wafuasi wa chama hicho wanaomuunga mkono katibu mkuu huyo.


Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, amedai kushangazwa na nguvu kubwa inayotumiwa na polisi katika kuzuia mikutano ya ndani inayoandaliwa na wafuasi wa chama hicho wanaomuunga mkono huku wakiruhusu inayoandaliwa na mwenyekiti wa chama hicho Profesa Ibrahim Lipumba.

“Mpaka muda ninavyoongea na nyinyi waandishi wa habari gari iliyokuwa kituoni kama kielelezo au sahihi limeondolewa kituoni hapo na watuhumiwa wote wameachiwa huru na wapo mitaani huku wakitamba wanalindwa na jeshi la polisi. Wamekuwa wakitisha katika mitandao ya kijamii na katika mazingira ambapo wapo wanachama wa CUF bila ya hofu kwani wanaamini na kusema waziwazi kwamba jeshi la polisi ni sehemu yao na haliwafanyi lolote,” alisema Seif.

Aidha Maalif Seif alisema kuwa suala la kuachiwa huru watuhumiwa wa utekaji nyara wa viongozi na wanachama wa CUF ni ukiukaji wa haki na kumtaka waziri wa mambo ya ndani Mwigulu Nchemba kuingilia kati.

DOWNLOAD APP YETU YA SWAHIBA NEWS ILI UWEZE KUPATA HABARI ZOTE MOJA KWA MOJA KUPITIA SIMU YAKO YA MKONONI BILA KUINGIA KWENYE WEBSITE,KUDOWNLOAD BONYEZA HAPA  

ANDIKA MAONI YAKO HAPO CHINI
 
ads
Bonyeza HAPA kudownload applicationi ya SWAHILI NEWS kwenye simu yako ili kupata habari zetu Haraka
Share To:

SWAHIBA MEDIA STAFF

Habari , karibu katika mtandao wetu ili kuhabarika na stori zote za siku katika lugha yetu adhwim ya kiswahili, habarika wakati wote weka dunia kiganjani mwako na swahili news

Post A Comment: