ads

Serikali ya Zambia imewataka watendaji wake na wale wa Tanzania kuchapa kazi na kuacha kupiga soga ili kuinua uchumi wa nchi hizo.


Rais wa nchi hiyo, Edgar Lungu amesema hayo wakati wa kuhitimisha ziara yake ya siku tatu baada ya kutembelea Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA) na Shirika la Kusafirisha na Kupokea Mizigo la Zambia (Zamcargo).

Amesema licha ya kuenzi mchango wa waasisi wa mataifa hayo, Mwalimu Julius Nyerere na Kenneth Kaunda, watajikita zaidi kwenye biashara.

“Changamoto mliyonayo ni kwenu uongozi na Bodi ya TPA kwa watu wa Kusini au Mashariki au hata nje ya Afrika. Watu wa Zambia wanasema muda wa siasa umekwisha, sasa ni muda wa maendeleo. Hatutawaunga mkono kwa sababu niko karibu sana na Rais (John) Magufuli. Ni kweli niko karibu na Rais Magufuli kama mlikuwa hamjui, lakini hatuwaungi mkono kwa sababu hiyo, bali kwa ufanisi wenu,” amesema Rais Lungu.

Akizungumzia miradi ya reli ya Tazara na bomba la mafuta la Tazama, Rais Lungu amesema nayo inapaswa kufanya kazi kwa ufanisi.

“Ni kweli sisi ni ndugu lakini hatuangalii hilo. Wazambia wanataka mbolea ifike haraka, shaba isafirishwe haraka kwenda sokoni,” amesema.

Awali, Mkurugenzi Mkuu wa TPA, Deusdedit Kakoko amesema mwaka 2014, Zambia ilichangia asilimia 36 ya mizigo ambayo ni sawa na tani milioni 5.2 ikiwa  ni mbali ya nchi nane zinazotumia bandari hiyo.

“Kwa mfano muda wa kutoa mizigo bandarini umepunguzwa hadi siku kumi na moja mwisho wa Oktoba kulinganisha na siku 32 zilizokuwa mwaka 2008. Bandari pia imeboresha mfumo wa malipo ya mizigo kwa wateja wake kwa kutumia mfumo wa kielektroniki,” amesema Kakoko.

Mara baada ya ziara hiyo, Rais Magufuli amewaongoza viongozi wengine wa Serikali kumsindikiza mgeni wake huyo uwanja wa ndege na kurejea Zambia.
DOWNLOAD APP YETU YA SWAHIBA NEWS ILI UWEZE KUPATA HABARI ZOTE MOJA KWA MOJA KUPITIA SIMU YAKO YA MKONONI BILA KUINGIA KWENYE WEBSITE,KUDOWNLOAD BONYEZA HAPA  

ANDIKA MAONI YAKO HAPO CHINI
ads
Bonyeza HAPA kudownload applicationi ya SWAHILI NEWS kwenye simu yako ili kupata habari zetu Haraka
Share To:

SWAHIBA MEDIA STAFF

Habari , karibu katika mtandao wetu ili kuhabarika na stori zote za siku katika lugha yetu adhwim ya kiswahili, habarika wakati wote weka dunia kiganjani mwako na swahili news

Post A Comment: