ads

Matokeo ya Uchaguzi Mkuu wa mwaka jana bado yanaiumiza Chadema ambayo imesema haitakubali yaliyotokea yajirudie katika uchaguzi ujao.


Katika uchaguzi huo, chama hicho kilishika nafasi ya pili nyuma ya CCM lakini kililalamikia matokeo huku kikisema kulikuwa na ukiukwaji wa taratibu na sheria za uchaguzi.

Rais John Magufuli alishinda uchaguzi huo kwa kupata kura 8,882,935, huku mpinzani wake, Edward Lowassa wa Chadema akipata kura 6,072,848.

Katibu Mkuu wa Chadema, Dk Vincent Mashinji amesema chama hicho hakitakubali kudhulumiwa kwa namna yoyote ile ushindi.

“Hii inaonyesha katika nchi yetu bado kuna tatizo la utendaji haki. Wewe umefanya mara ya kwanza, tukanyamaza, ukafanya tena mara ya pili tena kwa ubabe, tukalalamika, badala ya kusema njooni tuongee, unasema nendeni kokote. Sawa, tusubiri awamu ya tatu. Tukishindwa tutakupongeza, lakini tukishinda shughuli yake itakuwa ngumu,” amesema.

Kuhusu utawala wa Rais Magufuli, Dk Mashinji amesema kumekuwa na ukiukwaji wa utawala bora na matokeo yake yeye ndiyo amekuwa kila kitu.

“Wakati anaanza mapambano dhidi ya rushwa tuliamini angeweza kuliondosha tatizo hili, lakini hali ikawa tofauti,” amesema.

Amesema kadri siku zinavyokwenda, Serikali imeshindwa mapambano dhidi ya rushwa.

Pia, amesema katika mwaka mmoja huo wa Magufuli  ameshindwa kusimamia utawala bora baada ya kupiga marufuku mikutano ya hadhara na shughuli zote za siasa nchini kwa kile alichosema kuwa muda wa siasa umekwisha.

“Tuliposema hivi, watu wengi hawakutuelewa, lakini wakati anatuzuia tusifanye siasa, watu wengi walisema wale wanasiasa wamezidi,” amesema.
DOWNLOAD APP YETU YA SWAHIBA NEWS ILI UWEZE KUPATA HABARI ZOTE MOJA KWA MOJA KUPITIA SIMU YAKO YA MKONONI BILA KUINGIA KWENYE WEBSITE,KUDOWNLOAD BONYEZA HAPA  

ANDIKA MAONI YAKO HAPO CHINI
ads
Bonyeza HAPA kudownload applicationi ya SWAHILI NEWS kwenye simu yako ili kupata habari zetu Haraka
Share To:

SWAHIBA MEDIA STAFF

Habari , karibu katika mtandao wetu ili kuhabarika na stori zote za siku katika lugha yetu adhwim ya kiswahili, habarika wakati wote weka dunia kiganjani mwako na swahili news

Post A Comment: