ads

Katibu Mkuu wa Chadema, Dk Vincent Mashinji ameizungumzia operesheni Umoja wa Kupinga Udikteta Tanzania (ukuta) ambayo ilifanyiwa figisu kadhaa wakati wa utekelezaji wake hadi chama hicho kikaamua kuiweka kando kwa muda.


Dk Mashinji amesema mikutano na maandamano ilikuwa moja ya mikakati ya kufanikisha Ukuta.

“Sisi tulipotangaza Ukuta, tulitangaza mchakato kwa kuunda kamati ambazo ni pamoja na ya mawasiliano kueleza Ukuta ni nini; kamati inayowasiliana na wadau wa nje kama vile vyama vya wafanyakazi, wadau wa nje ya nchi; kamati iliyokuwa ikiratibu matukio ambayo sasa ndiyo hiyo waliyotegemea maandamano na mikutano,” amesema.

“Kuna kamati iliyokuwa ikihusika na mashauriano ya mikakati vikiwemo vyombo vya habari na kamati ya sheria.Unapopinga kitu chochote unapitisha ujumbe kwa wananchi ili wapate maana ya Ukuta.”

“Kwa hiyo Ukuta ni mwenendo wa maisha na ni endelevu siyo wa kuishia Septemba 1, ilikuwa ni kujipanga tu. Tulitumia neno ‘defiance’ ambalo wenzetu walilitafsiri kama uhaini, kitu ambacho siyo sawa,” amefafanua.

“Kwanza tulifanikiwa kupeleka tafsiri kwa watu. Wengi sasa wameshaelewa udikteta ni nini. Watu wanadhani demokrasia ni kufanya uchaguzi tu, demokrasia ni pana, uchaguzi ni sehemu tu. Ni pamoja na kusikilizwa, pamoja na kutoingiliwa uhuru wa mtu binafsi, ndiyo maana sisi tunasema Ukuta ulifanikiwa sana,” amesema Dk Mashinji.

Akizungumzia sababu za kuahirishwa kwa utekelezwaji wa Ukuta, Dk Mashinji amesema kulikuwa na sababu za msingi ikiwa pamoja na kuwaheshimu viongozi wa dini waliokuwa wakitafuta suluhu.

“Sasa kama viongozi wa dini wanasema, hili jambo mnalofanya ni zuri na sisi tumeliona, tunaomba tukamweleze bwana mkubwa nini kinaendelea. Sasa swali linakuja, kama wewe umesimama kwenye viatu vyetu, utaendelea au utaacha? Sisi kwa busara ya kawaida tuliona tuwasikilize,” amesema.

DOWNLOAD APP YETU YA SWAHIBA NEWS ILI UWEZE KUPATA HABARI ZOTE MOJA KWA MOJA KUPITIA SIMU YAKO YA MKONONI BILA KUINGIA KWENYE WEBSITE,KUDOWNLOAD BONYEZA HAPA  

ANDIKA MAONI YAKO HAPO CHINI
ads
Bonyeza HAPA kudownload applicationi ya SWAHILI NEWS kwenye simu yako ili kupata habari zetu Haraka
Share To:

SWAHIBA MEDIA STAFF

Habari , karibu katika mtandao wetu ili kuhabarika na stori zote za siku katika lugha yetu adhwim ya kiswahili, habarika wakati wote weka dunia kiganjani mwako na swahili news

Post A Comment: