ads

Miss Tanzania 2016, Diana Edward ametangaza vipaumbe vyake  kuwa ni kupinga ukeketaji, mila potofu na ndoa za utotoni hasa kwenye jamii za Kimasai na nyinginezo.


Mrembo huyo wa Kinondoni, Diana alitwaa taji la Miss Tanzania 2016, usiku wa kuamkia Jumapili kwenye Ukumbi wa Rock City Mall jijini Mwanza.

 Diana alinyakua taji hilo na kujitwalia gari aina ya Toyota IST na kitita cha Sh4 milioni baada ya kuwashinda warembo wenzake 29 kutoka mikoa mbalimbali nchini waliokuwa wakichuana kuwania taji hilo.

Akizungumza baada ya kutwaa taji hilo, Diana alisema haikuwa kazi rahisi kwani ushindani ulikuwa mkali ni mapenzi ya Mungu kumpa nafasi hiyo.

DOWNLOAD APP YETU YA SWAHIBA NEWS ILI UWEZE KUPATA HABARI ZOTE MOJA KWA MOJA KUPITIA SIMU YAKO YA MKONONI BILA KUINGIA KWENYE WEBSITE,KUDOWNLOAD BONYEZA HAPA  

ANDIKA MAONI YAKO HAPO CHINI
ads
Bonyeza HAPA kudownload applicationi ya SWAHILI NEWS kwenye simu yako ili kupata habari zetu Haraka
Share To:

SWAHIBA MEDIA STAFF

Habari , karibu katika mtandao wetu ili kuhabarika na stori zote za siku katika lugha yetu adhwim ya kiswahili, habarika wakati wote weka dunia kiganjani mwako na swahili news

Post A Comment: