ads

KIONGOZI Mkuu wa chama cha ACT-Wazalendo, Kabwe Zitto, amemuunga mkono Rais John Magufuli, kwa kuwakataza wafuasi wote wa chama hicho, kutojihusisha na maandamano ya aina yoyote kwa kuwa chama hicho hakijatangaza maandamano.


Kauli hiyo ya Zitto, imekuja siku moja baada ya Rais Magufuli kuonya kuwa atakayethubutu kuandamana atakiona cha mtema kuni, huku Naibu Katibu Mkuu wa Chadema Zanzibar, Salum Mwalimu, akitangaza kuwa maandamano ya wafuasi wa chama hicho nchi nzima, yako pale pale.

Katika taarifa yake aliyotoa jana kwa vyombo vya habari, Zitto amesisitiza kwa wanachama hao na wafuasi wa chama hicho, kutojihusisha na maandamano ya aina yoyote kwa kuwa chama hicho hakijatangaza maandamano.

Katika hatua nyingine Zitto amewataka wafuasi hao, kutoona aibu kuunga mkono uamuzi wowote wa serikali au chama chochote cha siasa, unaoendana na azimio la Tabora hususan katika vita dhidi ya ufisadi na kurejeshwa kwa miiko ya uongozi.

“Tuwe mstari wa mbele kupinga ufisadi kwani rushwa ni adui wa haki. Tuwe mstari wa mbele kutaka kurejeshwa kwenye miiko ya uongozi, sisi ndiyo chama pekee chenye itikadi iliyo wazi, tuisimamie popote tulipo bila woga wala aibu,” ilieleza taarifa hiyo.

Katika taarifa yake hiyo, Zitto amewataka wanachama wa chama hicho kusoma, kuelewa na kujadili Azimio la Tabora na kuchambua muktadha wake katika mazingira ya sasa ya siasa za nchini, kwa kuwa chama hicho kiliundwa kwa madhumuni ya kurejesha nchi kwenye misingi yake.

Kuandika barua

Aidha, ameagiza kila mwanachama wa chama chake aandike barua kwa Rais Magufuli kwa namna anavyoona yeye kumtaka alichodai kuacha kuingiza nchi kwenye utawala wa imla.

“Chama chetu kina wanachama 431,120 wenye kadi, Ikulu ikipata barua 200,000 kutoka kila kona ya nchi itafunguka macho,” ilidai taarifa hiyo.

DOWNLOAD APP YETU YA SWAHIBA NEWS ILI UWEZE KUPATA HABARI ZOTE MOJA KWA MOJA KUPITIA SIMU YAKO YA MKONONI BILA KUINGIA KWENYE WEBSITE,KUDOWNLOAD BONYEZA HAPA  

ANDIKA MAONI YAKO HAPO CHINI

ads
Bonyeza HAPA kudownload applicationi ya SWAHILI NEWS kwenye simu yako ili kupata habari zetu Haraka
Share To:

SWAHIBA MEDIA STAFF

Habari , karibu katika mtandao wetu ili kuhabarika na stori zote za siku katika lugha yetu adhwim ya kiswahili, habarika wakati wote weka dunia kiganjani mwako na swahili news

Post A Comment: