ads

RAIS John Magufuli, ametengua uteuzi wa Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Bagamoyo, Azimina Mbilinyi ambaye amehudumu katika cheo hiko kwa siku 24 tu.


Taarifa ya Ikulu iliyotumwa jana kwa vyombo vya habari na Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi), Musa Iyombe, imesema kuwa Rais hajaridhishwa na utendaji wake.

Ingawa taarifa hiyo haikufafanua zaidi, lakini wakati wakurugenzi hao walipokuwa wakila Kiapo cha Uadilifu wa Uongozi wa Umma katikati ya mwezi huu, Rais Magufuli alisema kila mkurugenzi aliyechaguliwa, atambue kuwa sifa zake zilichambuliwa na Rais mwenyewe.
Azimina Mbilinyi,aliyekuwa Mkurugenzi Bagamoyo

Hata hivyo, aliwataka kuhakikisha wanasimamia vyema fedha za serikali zinazowasilishwa katika halmashauri na kuepuka kuburuzwa, kujipendekeza, kukejeliwa au kutumika vibaya kwa kuingia mikataba na kampuni feki zisizoweza kutekeleza vyema wajibu wake.

Magufuli alisema anazo taarifa za baadhi ya wakurugenzi, walikuwa wakishirikiana na mameya, madiwani na wenyeviti wa halmashauri kwa kupitisha na kuingia mikataba na kampuni zilizo na uwezo chini ya viwango katika kutekeleza miradi ya barabara na matokeo yake miradi mingi haikuwa na mafanikio.

DOWNLOAD APP YETU YA SWAHIBA NEWS ILI UWEZE KUPATA HABARI ZOTE MOJA KWA MOJA KUPITIA SIMU YAKO YA MKONONI BILA KUINGIA KWENYE WEBSITE,KUDOWNLOAD BONYEZA HAPA  


ANDIKA MAONI YAKO HAPO CHINI

ads
Bonyeza HAPA kudownload applicationi ya SWAHILI NEWS kwenye simu yako ili kupata habari zetu Haraka
Share To:

SWAHIBA MEDIA STAFF

Habari , karibu katika mtandao wetu ili kuhabarika na stori zote za siku katika lugha yetu adhwim ya kiswahili, habarika wakati wote weka dunia kiganjani mwako na swahili news

Post A Comment: