ads

Wanachama wa klabu ya Simba wanakutana katika mkutano mkuu wa klabu hiyo utakaofanyika kwenye Bwalo la Maofisa wa Polisi, Oysterbay, Dar es Salaam leo.


Licha ya kuwapo na agenda mbalimbali ikiwamo ya usajili, mapato na matumizi ya klabu na maendeleo ya klabu, suala kubwa linalotarajia kuibua mvutano ni uwekezaji wa Mfanyabiashara Mohamed Dewji ‘MO’ aliyepanga kuwekeza Sh20bilioni katika klabu hiyo.

Uzoefu wa klabu za Simba na Yanga, viongozi hubanwa hasa eneo la mapato na matumizi ya klabu, lakini safari hii linaonekana kutokuwa na nguvu zaidi ya suala la uwekezaji wa MO klabuni hapo.

Suala hilo ndilo linalofanya wanachama na mashabiki wa Simba kuzozana kila mahali huku kila mmoja akitoa hoja kwa kadri ya upeo wake kuhusu uwekezaji huo.

Baadhi ya wanachama wa Simba walisema wanatarajia kila hoja itakayowasilishwa katika mkutano wa leo itapewa uzito unaostahili ili kuhakikisha Simba inakuwa na umoja na kupata mafanikio.

DOWNLOAD APP YETU YA SWAHIBA NEWS ILI UWEZE KUPATA HABARI ZOTE MOJA KWA MOJA KUPITIA SIMU YAKO YA MKONONI BILA KUINGIA KWENYE WEBSITE,KUDOWNLOAD BONYEZA HAPA  

ANDIKA MAONI YAKO HAPO CHINI
ads
Bonyeza HAPA kudownload applicationi ya SWAHILI NEWS kwenye simu yako ili kupata habari zetu Haraka
Share To:

SWAHIBA MEDIA STAFF

Habari , karibu katika mtandao wetu ili kuhabarika na stori zote za siku katika lugha yetu adhwim ya kiswahili, habarika wakati wote weka dunia kiganjani mwako na swahili news

Post A Comment: