ads

BAADA ya Chadema inayoongoza vyama vinavyounda Ukawa, kuzunguka huku na huko ikiwemo kususa Bunge na kufanya uchochezi, huku maonyo mbalimbali yakitolewa, hatimaye Rais John Magufuli, ametoa karipio la mwisho.


Wiki hii Chadema baada ya kumaliza kikao chake cha Kamati Kuu, ikiongozwa na Mwenyekiti wake, Freeman Mbowe, ilitangaza kuanza ilichoita operesheni ya Umoja wa Kupinga Udikteta Tanzania (Ukuta), itakayofanyika kwa mikutano ya hadhara, itakayotanguliwa na maandamano nchi nzima, kupinga huo udikteta na utawala kandamizi.

“Wasinijaribu kwa kulazimisha maandamano siku ya tarehe moja Septemba...atakayethubutu kufanya hivyo, kitakachompata mmmh, hatasahau kamwe. Mimi ni tofauti sana, wasije wakanijaribu.

“Sitaki nchi hii iwe ya vurugu, watakaoleta vurugu mimi nitawashughulikia kikamilifu bila huruma ...kama wapo watu wanaowatumia wakawaeleze vizuri, mimi sijaribiwi na wala sitajaribiwa. Wananchi hawa wana shida na siasa nzuri ni wananchi washibe, siasa nzuri ni wananchi wetu wapate dawa,” ameonya Rais Magufuli.

Onyo la mwisho

Katika onyo la mwisho alilotoa Rais Magufuli jana, alianza kwa kufafanua kwamba hajapiga marufuku wanasiasa kufanya mikutano ya kuhimiza maendeleo kwenye maeneo yao.

“Kama wewe ni Mbunge wa Jimbo la Hai (kwa sasa Freeman Mbowe), zunguka kwenye jimbo lako hadi uchoke, si unaacha kwako unaenda Shinyanga kushawishi watu waandamane. Mimi sijazuia shughuli za waliochaguliwa kwenye maeneo yao, bali nimekataa mtu kuondoka jimboni kwake na kwenda kufanya fujo mahali pengine,” alionya.

Ukaidi wa Chadema

Katika kudhihirisha ukaidi wao, Chadema jana iliitisha mkutano na vyombo vya habari, ambapo katika muendelezo wa siasa hizo, Naibu Katibu Mkuu wake Zanzibar, Salum Mwalimu, alisisitiza kuwa azma yao ya kufanya mikutano yake ya hadhara nchi nzima, kuanzia Septemba mosi mwaka huu iko pale pale.

“Tumewaita hapa kwanza kusisitiza azma yetu ya Septemba mosi kuwa ni siku ya kukataa udikteta, utawala kandamizi na ukandamizaji iko pale pale, hatutarudi nyuma, hatutishiki na hatutetereki,” alisema Mwalimu.

DOWNLOAD APP YETU YA SWAHIBA NEWS ILI UWEZE KUPATA HABARI ZOTE MOJA KWA MOJA KUPITIA SIMU YAKO YA MKONONI BILA KUINGIA KWENYE WEBSITE,KUDOWNLOAD BONYEZA HAPA  

ANDIKA MAONI YAKO HAPO CHINI
ads
Bonyeza HAPA kudownload applicationi ya SWAHILI NEWS kwenye simu yako ili kupata habari zetu Haraka
Share To:

SWAHIBA MEDIA STAFF

Habari , karibu katika mtandao wetu ili kuhabarika na stori zote za siku katika lugha yetu adhwim ya kiswahili, habarika wakati wote weka dunia kiganjani mwako na swahili news

Post A Comment: