ads

TAASISI ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru), imeanza kuchunguza kashfa ya Sh. bilioni 60 inayolikabili Jeshi la Polisi baada ya kuibuliwa na Rais John Magufuli hivi karibuni.


Rais Magufuli aliibua kashfa hiyo wakati akiwaapisha Naibu Makamishna wa Polisi (DCP) na Makamishna Wasaidizi Waandamizi wa Polisi (SACP) baada ya kuwapandisha vyeo na kula kiapo cha uadilifu wa utumishi wa umma, Julai 18, mwaka huu Ikulu, jijini Dar es Salaam.

Kuhusu kashfa hiyo, Rais Magufuli alieleza kuwa mwishoni mwa mwaka jana kuna mtu ndani ya Jeshi la Polisi alipewa kazi ya kununua sare za Jeshi la Polisi na kupewa fedha lakini hakutimiza wajibu huo hadi mwaka huu.

“Naomba suala hili lifuatiliwe, wapo wanaosema fedha zilizotolewa zilikuwa Sh. bilioni 20, wengine Sh. bilioni 60, kwa hiyo Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Ndani, Meja Jenerali Projest Rwegasira wewe ni mwanasheria, waliohusika wapelekwe mbele ya haki,” alisema Rais Magufuli.

Akizungumza na Nipashe jana kwa simu, Mkurugenzi Mkuu wa Takukuru, Kamishna Valentino Mlowola, alisema suala hilo walianza kulifanyia kazi tangu walipopata taarifa.

Alisema hadi sasa uchunguzi unaendelea kuhusu suala hilo kwani tuhuma zozote zenye viashiria vya rushwa zinapotokea hufanyiwa kazi mara moja na taasisi hiyo.

“Zoezi hili tulilianza siku ileile aliyosema Rais, uchunguzi unaendelea kuhusu suala hilo, na uchunguzi wowote utakaousikia wewe uwe wa kiuchumi, kijamii au kisiasa sisi tunaufanyia kazi,” alisema Mlowola.

DOWNLOAD APP YETU YA SWAHIBA NEWS ILI UWEZE KUPATA HABARI ZOTE MOJA KWA MOJA KUPITIA SIMU YAKO YA MKONONI BILA KUINGIA KWENYE WEBSITE,KUDOWNLOAD BONYEZA HAPA  

ANDIKA MAONI YAKO HAPO CHINI


ads
Bonyeza HAPA kudownload applicationi ya SWAHILI NEWS kwenye simu yako ili kupata habari zetu Haraka
Share To:

SWAHIBA MEDIA STAFF

Habari , karibu katika mtandao wetu ili kuhabarika na stori zote za siku katika lugha yetu adhwim ya kiswahili, habarika wakati wote weka dunia kiganjani mwako na swahili news

Post A Comment: