ads

Waziri wa Mambo ya Ndani, Mwigulu Nchemba, amefanya ziara ya kushtukiza katika Mgodi wa Dhahabu wa Nyamahuna mkoani  Geita na kukuta Wachina 72 kati ya 100 wakiishi na kufanya kazi bila vibali.


Akizungumza katika mgodi huo unaomilikiwa na Mtanzania, Andrew Obole, Mwigulu alisema alifika hapo kutokana na kuona taarifa zilizozagaa kwenye mitandao ya jamii.

Mwigulu alisema taarifa hizo zilimuonyesha Masanja Shokera akicharazwa bakora na raia wa mmoja wa China, Lee Swii, kwa madai ya kuiba mawe ya dhahabu Julai 6, mwaka huu.

“Nimefika kuthibitisha nilichokisikia kwamba kuna raia wa kigeni wanachapa watu hapa. Nimemuona mtuhumiwa wa udhalilishaji na kushangazwa na kukuta wafanyakazi wa China hapa wapatao 100 kwenye mgodi huo,” alisema.

Alisema taarifa alizonazo ambazo zipo uhamiaji zinaonyesha kuwa raia wa China waliopo mgodini hapo ni 28 ambao wana vibali halali vya kuishi nchini.

Waziri alisema kwa sababu hiyo, aliagiza Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa wa Geita kuwaweka chini ya ulinzi Wachina wengine 72, walinzi saba   na Kaimu Meneja Uzalishaji, Richard Joachim.

“Wakati hawa wakiwa chini ya ulinzi  naiagiza Kamati ya Ulinzi na Usalama Mkoa wa Geita kuchunguza uhalali wa raia hao wa China kuishi nchini bila ya kuwa na vibali.

Vilevile  huyo anayeitwa Lee ambaye anatuhumiwa kumdhalilisha Mtanzania mwenzetu awekwe chini ya ulinzi na walinzi saba na kumpiga na kumjeruhi,”alisema.

Masanja Shokera ambaye anayedaiwa  kudhalilishwa,  , alisema  siku hiyo alivamiwa na walinzi wa mgodi huo  akituhumiwa kuiba mawe ya dhahabu.

Alisema walimpiga  na kumfunga mikono na miguu na kuendelea kumwadhibu hali iliyosababisha apoteze fahamu.

“Walionipiga wote nawatambua, ni hawa walinzi wa Kimasai wote walinishambulia na huyu Mchina alikuja pia kunipiga wakati nimefungwa kamba… alianza huyu mkuu wa ulinzi,  Sitta Dotto kuwaamrisha nikaguliwa kunipiga kichwani,” alisema.

Mkurugenzi wa mgodi huo, Andrew Obole    alisema anachotambua Wachina waliopo kwake ni 28 na kwamba hao wengine alikuwa hawatambui.

DOWNLOAD APP YETU YA SWAHIBA NEWS ILI UWEZE KUPATA HABARI ZOTE MOJA KWA MOJA KUPITIA SIMU YAKO YA MKONONI BILA KUINGIA KWENYE WEBSITE,KUDOWNLOAD BONYEZA HAPA  

ANDIKA MAONI YAKO HAPO CHINI


ads
Bonyeza HAPA kudownload applicationi ya SWAHILI NEWS kwenye simu yako ili kupata habari zetu Haraka
Share To:

SWAHIBA MEDIA STAFF

Habari , karibu katika mtandao wetu ili kuhabarika na stori zote za siku katika lugha yetu adhwim ya kiswahili, habarika wakati wote weka dunia kiganjani mwako na swahili news

Post A Comment: