ads

WAKATI wadau wa soka nchini wameitaka Yanga kujipanga upya baada ya nafasi yao ya kusonga mbele katika mashindano ya Kombe la Shirikisho Afrika kuwa finyu, aliyekuwa Rais wa Simba,Ismail Aden Rage ameishauri klabu hiyo kujiuliza pale ilipokosea ili mwakani waweze kufanya vizuri kwenye michuano hiyo.


 Kauli hizo za wadau zimetolewa jana kufuatia Yanga kukubali kichapo cha mabao 3-1 kutoka kwa Medeama ya Ghana katika mechi yake ya nne ya Kundi A iliyofanyika juzi mjini Sekondi- Takoradi. 

Rage alisema kuwa Yanga inatakiwa kukubaliana na matokeo hayo na kuyafanyia kazi makosa yaliyojitokeza mwaka huu kutojirudia katika msimu ujao.

"Yanga wanatakiwa wajiulize ni kwanini wanafanya vizuri kwenye ligi ya ndani na mechi za kimataifa wanashindwa, je wanajiandaa zaidi na Ligi Kuu na kutofanya kipaumbele maandalizi ya mechi za kimataifa hadi inapelekea kufanya vibaya," alihoji Rage.

DOWNLOAD APP YETU YA SWAHIBA NEWS ILI UWEZE KUPATA HABARI ZOTE MOJA KWA MOJA KUPITIA SIMU YAKO YA MKONONI BILA KUINGIA KWENYE WEBSITE,KUDOWNLOAD BONYEZA HAPA  

ANDIKA MAONI YAKO HAPO CHINI

ads
Bonyeza HAPA kudownload applicationi ya SWAHILI NEWS kwenye simu yako ili kupata habari zetu Haraka
Share To:

SWAHIBA MEDIA STAFF

Habari , karibu katika mtandao wetu ili kuhabarika na stori zote za siku katika lugha yetu adhwim ya kiswahili, habarika wakati wote weka dunia kiganjani mwako na swahili news

Post A Comment: