ads


Hatimaye Kada maarufu wa Chadema na aliyekuwa Mgombea Urais wa UKAWA katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2015,Mhe Edward Lowassa leo hii ameamua kuvunja ukimya juu ya ukaribu wake na rafiki yake wa kipindi kirefu Dr Jakaya Kikwete.


Lowassa ambaye leo alifanya mahojiano na kituo kimoja cha Luninga,amesema kuwa baada ya tukio la kukatwa kwake wakati anawania nafasi ya Urais kupitia CCM,kisha kujiunga na Chadema hakupata nafasi ya kukutana na JK.
 

Itakumbukwa kuwa JK aliongoza kamati kuu ya Chadema kumkata Lowassa katika mkutano Mkuu wa CCM dodoma Mwaka jana.

Lowassa amesema kuwa hawezi kumuhukumu JK kwa tukio lile zaidi ya kumuachia mwenyewe ajihukumu.

Aidha katika hatua nyingine Lowassa amesema kuwa anampongeza Rais wa sasa Dr John Magufuli kwa kuanza vema,ila akadai kuwa kama angekuwa yeye angeweza kufanya vema zaidi ya Dr JPM.

Amesema kuwa JPM ameanza na suala la madawati lakini yeye angeanza na suala la kuboresha maslahi ya walimu kwanza ili kuinua kiwango cha Elimu.

Aidha amependekeza kuwa ni vema Rais Magufuli akawa anashauriwa ili kusudi kuhakikisha anaongoza vema,ikiwemo kuachana na tabia ya kuongoza nchi kwa imla.

Katika hatua nyingine Lowassa amesema kuwa anamshauri Rias Shein kutafuta njia muafaka ya maridhiano na CUF ili kuhakikisha usalama wa visiwa hivyo.

DOWNLOAD APP YETU YA SWAHIBA NEWS ILI UWEZE KUPATA HABARI ZOTE MOJA KWA MOJA KUPITIA SIMU YAKO YA MKONONI BILA KUINGIA KWENYE WEBSITE,KUDOWNLOAD BONYEZA HAPA  

ANDIKA MAONI YAKO HAPO CHINI

ads
Bonyeza HAPA kudownload applicationi ya SWAHILI NEWS kwenye simu yako ili kupata habari zetu Haraka
Share To:

SWAHIBA MEDIA STAFF

Habari , karibu katika mtandao wetu ili kuhabarika na stori zote za siku katika lugha yetu adhwim ya kiswahili, habarika wakati wote weka dunia kiganjani mwako na swahili news

Post A Comment: