ads
 
Mfanyabiashara Mohammed Dewji maarufu kama Mo, ametawala katika mkutano wa wanachama wa Simaba uliofanyika leo jijini Dar es Salaam.

Wanachama walionekana wazi kuwa wana hamu ya kuusikia uongozi wao unasema nini kuhusiana na kuingia kwenye kampuni ambako Simba itaweza kuuza hisa.

Uamuzi huo, ulisababisha wanachama kutotaka kujadili chochote zaidi ya kuona kama uongozi uko tayari kuuza hisa zake asilimia 51 kwa Sh bilioni 20 kwa Mo.

Wakati wa kujadili ajenda nyingine za kikao kama zile za Hesabu, Chombo cha uchaguzi na kadhalika, hazikuwa na mvuto na wengi walitaka ajenda namba tisa ambayo ilikuwa ni “Taarifa ya kamati ya maboresho ya mfumo wa uendeshaji”.

Lakini wanachama hao walianza kulalamika wakiona kama uongozi ulipita haraka hapo. Wakaanza kupiga kelele wakitaka kusikia mjadala.

Mwisho, Rais wa Simba Evans Avena alilazimika kurejea na kuwaeleza kwamba kama wanataka Simba kuingia kwenye mchakato wa kampuni, maoni yao yamesikilizwa na yanaanza kufanyiwa kazi.

Kauli hiyo ya Aveva, ilifanya wanachama hao washangilie kwa nguvu hata yeye baada ya kuufunga mkutano huo.
 
credit-salehjembe
 
DOWNLOAD APP YETU YA SWAHIBA NEWS ILI UWEZE KUPATA HABARI ZOTE MOJA KWA MOJA KUPITIA SIMU YAKO YA MKONONI BILA KUINGIA KWENYE WEBSITE,KUDOWNLOAD BONYEZA HAPA  

ANDIKA MAONI YAKO HAPO CHINI
 
ads
Bonyeza HAPA kudownload applicationi ya SWAHILI NEWS kwenye simu yako ili kupata habari zetu Haraka
Share To:

SWAHIBA MEDIA STAFF

Habari , karibu katika mtandao wetu ili kuhabarika na stori zote za siku katika lugha yetu adhwim ya kiswahili, habarika wakati wote weka dunia kiganjani mwako na swahili news

Post A Comment: