![ads](http://1.bp.blogspot.com/-J5aEnGVep5k/WJTrf2fzuPI/AAAAAAAAU5U/_iuE-DY1RHAM5_hqPHb-UuNbabG2xn2nwCK4B/s1600/AdvertiseHere.jpg)
KOCHA Mkuu wa mabingwa wa Ligi Kuu ya
Vodacom (VPL) Yanga Mdachi Hans van der Pluijm amesema kuwa kufanya
vibaya kwa timu yake katika michezo minne ya hatua ya makundi ya Kombe
la Shirikisho Afrika kumetokana na kikosi hicho kutokuwa na bahati
kwenye michuano hiyo.
Akizungumza jana, Pluijm alisema kuwa alikiandaa vizuri kikosi chake
kwa ajili ya kusaka ushindi lakini jambo hilo lilishindikana na
hatimaye imeambulia pointi moja katika mechi nne za Kundi A ambazo
wamecheza.
Pluijm alisema kuwa hata hivyo hajakata tamaa na wataendelea na maandalizi kwa ajili ya kuhakikisha wanapata matokeo mazuri katika mechi mbili zilizobakia kwa sababu anaamini kwenye soka lolote linaweza kutokea.
"Hatuko katika nafasi nzuri, tunachotakiwa kukifanya sasa ni kuhakikisha tunatoka hapa, tutajipanga kuhakikisha tunafanya kila linalowezekana ili kufufua matumaini," alisema Pluijm.
Mdachi huyo alisema kuwa kikosi chake kilikuwa na makosa kadhaa ambayo wapinzani wao waliyatumia kupata ushindi tofauti na inavyokuwa kwenye mechi za Ligi Kuu Bara.
"Wanafanya makosa ambayo katika mechi za Ligi Kuu hawafungwi, lakini katika mashindano haya ya kimataifa, timu zina uzoefu na kutumia nafasi hiyo kupata mabao, ni changamoto mpya ambayo tumekutana nayo kwenye michuano hii, tumejifunza na tutabadilika kwenye mechi zinazofuata," Pluijm alisema.
Aliongeza kuwa mbali na ushiriki wa michuano hiyo ya kimataifa, Yanga pia inajipanga kuikabili Azam FC katika mchezo wa Ngao ya Hisani unaotarajiwa kufanyika Agosti 17 mwaka huu kwenye Uwanja wa Taifa Dar es Salaam.
Kikosi cha Yanga ambacho kimesharejea nchini kikitokea Ghana, kitaanza mazoezi Jumatatu kwa ajili ya kuikaribisha Mo Bejaia ya Algeria wakati mchezo mwingine wa Kundi A utakuwa ni kati ya TP Mazembe ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) dhidi ya Medeama utakaochezwa Ghana.
Pluijm alisema kuwa hata hivyo hajakata tamaa na wataendelea na maandalizi kwa ajili ya kuhakikisha wanapata matokeo mazuri katika mechi mbili zilizobakia kwa sababu anaamini kwenye soka lolote linaweza kutokea.
"Hatuko katika nafasi nzuri, tunachotakiwa kukifanya sasa ni kuhakikisha tunatoka hapa, tutajipanga kuhakikisha tunafanya kila linalowezekana ili kufufua matumaini," alisema Pluijm.
Mdachi huyo alisema kuwa kikosi chake kilikuwa na makosa kadhaa ambayo wapinzani wao waliyatumia kupata ushindi tofauti na inavyokuwa kwenye mechi za Ligi Kuu Bara.
"Wanafanya makosa ambayo katika mechi za Ligi Kuu hawafungwi, lakini katika mashindano haya ya kimataifa, timu zina uzoefu na kutumia nafasi hiyo kupata mabao, ni changamoto mpya ambayo tumekutana nayo kwenye michuano hii, tumejifunza na tutabadilika kwenye mechi zinazofuata," Pluijm alisema.
Aliongeza kuwa mbali na ushiriki wa michuano hiyo ya kimataifa, Yanga pia inajipanga kuikabili Azam FC katika mchezo wa Ngao ya Hisani unaotarajiwa kufanyika Agosti 17 mwaka huu kwenye Uwanja wa Taifa Dar es Salaam.
Kikosi cha Yanga ambacho kimesharejea nchini kikitokea Ghana, kitaanza mazoezi Jumatatu kwa ajili ya kuikaribisha Mo Bejaia ya Algeria wakati mchezo mwingine wa Kundi A utakuwa ni kati ya TP Mazembe ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) dhidi ya Medeama utakaochezwa Ghana.
DOWNLOAD
APP YETU YA SWAHIBA NEWS ILI UWEZE KUPATA HABARI ZOTE MOJA KWA MOJA
KUPITIA SIMU YAKO YA MKONONI BILA KUINGIA KWENYE WEBSITE,KUDOWNLOAD
BONYEZA HAPA
ANDIKA MAONI YAKO HAPO CHINI
Post A Comment: