ads

Peter Msigwa, Mbunge wa Iringa mjini (Chadema) amemshauri Dk John Magufuli, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuuza kwanza Ikulu kabla ya kuuza majengo mengine ya serikali ili zipatikane hela za kuhamia Dodoma,


Msigwa amesema hayo kupitia ukurasa wake wa mtandao wa kijamii wa facebook na kusisitiza kuwa haamini kama watanzania ni kama ng’ombe wataswagwa swagwa tu.

“We have a serious challenge as a National(tunachangamoto hasa kama taifa), nimshauri Rais aanze kwanza kuuza Ikulu ndipo majengo mengine ya umaa yafuate, nadhani ikulu itapata wateja mapema , tutapata hela za kuhamia Dodoma.” Ilisomeka kauli ya Msigwa.

Mbunge huyo pia amesema haamini kuwa watanzania nikama ng’ombe ambao wataswagwa swagwa tu wakae kimya, na kuonya kuwa mengi watayaona ambayo bado hayajajiri.

Kauli ya Msigwa inakuja ikiwa ni wiki tu tangu serikali ya Magufuli kutangaza mpango wake wa kuhamishia serikali yote mkoani Dodoma kabla ya mwaka 2020.

Magufuli alitoa kauli hiyo, wakati akihutubia mkutano mkuu maalum wa chama chake – Chama Cha Mapinduzi (CCM) – tarehe 23 Julai. Mkutano mkuu wa CCM uliomalizika mkoani Dodoma wiki iliyopita, ulimchagua Dk. Magufuli, kuwa mwenyekiti wa tano wa chama hicho.

Katika hotuba yake mbele ya wajumbe, Magufuli ameeleza kile alichoita, “dhamira yake ya dhati ya kukamilisha mpango wa serikali wa kuhamia Dodoma.”


DOWNLOAD APP YETU YA SWAHIBA NEWS ILI UWEZE KUPATA HABARI ZOTE MOJA KWA MOJA KUPITIA SIMU YAKO YA MKONONI BILA KUINGIA KWENYE WEBSITE,KUDOWNLOAD BONYEZA HAPA  

ANDIKA MAONI YAKO HAPO CHINI
ads
Bonyeza HAPA kudownload applicationi ya SWAHILI NEWS kwenye simu yako ili kupata habari zetu Haraka
Share To:

SWAHIBA MEDIA STAFF

Habari , karibu katika mtandao wetu ili kuhabarika na stori zote za siku katika lugha yetu adhwim ya kiswahili, habarika wakati wote weka dunia kiganjani mwako na swahili news

Post A Comment: